Tuesday, March 10, 2020

DKT. NDUMBARO AFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WA PALESTINA NA USWISI NCHINI


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli Pamoja na Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher, katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo ya Mhe. Dkt. Ndumbaro pamoja na Balozi wa Palestina, Mhe. Balozi Abuali walikubaliana kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi hasa katika sekta ya uwekezaji wa kiwanda cha dawa na vifaa tiba pamoja na kilimo.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Dkt. Ndumbaro na Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher mazungumzo yao yalihusu maandalizi ya mpango mpya wa maendeleo wa mwaka 2021-2024 baina ya Tanzania na Uswisi yanayoendelea.

Mpango wa maendeleo uliopo unatarajiwa kufikia ukomo mwaka huu 2020. Ambapo mpango mpya utajikita zaidi katika kuimarisha sekta ya afya, mazingira, utawala bora na kukuza ajira kwa vijana na wanawake nchini.

Masuala mengine yaliyojadiliwa yalihusu programu ya Ukuzaji Ujuzi wa Ajira nchini (Skills for Employment Tanzania) na shuguli zinazofanywa na NGOs za Uswisi zilizopo nchini.

Pia Kaimu Balozi huyo alieleza kuwa Uswisi itaendelea kusaidia mradi wa malaria na kuchangia fedha katika Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Kwa upande wake Mhe. Dkt. Ndumbaro alisifu uhusiano baina ya nchi hizi mbili kwa kueleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Uswisi katika kukuza zaidi mahusiano hayo.


Balozi wa Palestina Nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli akimuelezea jambo Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiongea na Balozi wa Palestina Nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher akiongea na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akimfafanulia jambo Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher wakati wa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.