Tuesday, March 31, 2020

PROF. KABUDI ATEMBELEA IDARA NA VITENGO WIZARANI AZUNGUMZA NA WATUMISHI



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof.  Palamagamba John Kabudi (wa kwanza kulia) akizungumza na watumishi wa Idara ya Ulaya na Amerika wakati alipowatembelea na kujadililiana nao masuala mbalimbali ya utendaji kazi wa Idara hiyo kwenye ofisi za Wizara zilizopo Chuo Kikuu cha Dodoma, tarehe 31 Machi 2020

Mhe. Waziri Prof. Kabudi akimsikiliza mmoja wa watumishi wa Idara ya  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakitoa ufafanuzi kuhusiana na utekelezaji wa majukumu ya idara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof.  Palamagamba John Kabudi ametembelea Idara na vitengo vya wizarani na kuzungumza na watumishi walioko katika ofisi za wizara
kwenye majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma, tarehe 31 Machi 2020.

Prof. Kabudi ametumia nafasi hiyo kuzungumza na mtumishi mmoja mmoja ili kuwafahamu na kuona jinsi  wanavyoyafahamu na kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kuona namna wanavyogeuza changamoto wanazokutana nazo kuwa fursa katika sehemu zao za kazi


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.