Friday, March 18, 2022

Balozi Possi Afanya Ziara ya Kikazi Jamhuri ya Czech

Balozi Possi Afanya Ziara ya Kikazi Jamhuri Czech

Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Czech mwenye makazi yake Berlin, Ujerumani, Dkt. Abdallah Possi amefanya ziara ya kikazi katika nchi ya Jamhuri ya Czech na kufanya mazungumzo na Naibu Mawaziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Miloslav Stašek; Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Jakub Dvořáček na Naibu Waziri wa Elimu, Mhe. Prof. Jaroslav Miller tarehe 17 Machi 2022.

Wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dkt. Possi aliwasilisha ombi ili Watanzania waweze kunufaika na Mpango wa Nafasi za Ufadhili wa Masomo unaoratibiwa na Wizara hiyo. Kwa sasa, nchi za Africa zinazonufaika na mpango huo ni Zambia na Ethiopia. Mhe, Naibu Waziri aliahidi kulifanyia kazi ombi hilo. Aidha, Mhe. Stašek aliwasilisha mualiko wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kufanya ziara ya kikazi Jamhuri ya Czech.

Katika mazungumzo yake na Naibu Waziri wa Afya, Balozi Possi aliomba Serikali ya nchi hiyo kuangalia uwezekano wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika sekta ya Afya, hususan katika magonjwa ya moyo na figo. Serikali ya Jamhuri ya Czech imeahidi kulifanyia kazi ombi hilo na kuahidi pia kuwa ipo tayari kuisaidia Tanzania dozi za chanjo ya UVIKO-19.

Kwa upande wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Elimu, wawili hao walijadili kuhusu ushirikiano wa Vyuo Vikuu, na namna ambavyo wanafunzi wa Tanzania waliokatiza masomo nchini Ukraine wanaweza kurahisishiwa mchakato wa kuhamisha alama na kumalizia masomo yao katika vyuo vikuu vya Czech.  Prof. Miller alimweleza Balozi Dkt. Possi wataanza na utaratibu wa awali wa kuvitaarifu vyuo vikuu vya Czech na kutoa kipaumbele kwa wanafunzi wa Tanzania, huku taratibu nyingine za kiufundi zikifuata.

Mhe. Miller aliahidi pia kuwa mamlaka husika zitaweka tangazo katika tovuti ya “Study in Czech Republic” ili  kuwahamasisha wanafunzi wa Tanzania waliokuwa Ukraine kuomba kujiunga na vyuo vikuu Jamhuri ya Czech.

 

Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Czech mwenye makazi yake Berlin, Ujerumani, Mhe. Dkt. Abdallah Possi akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe.Miloslav Stašek walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi zao.

Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Czech mwenye makazi yake Berlin, Ujerumani, Mhe. Dkt. Abdallah Possi akisalimiana na Naibu Waziri wa Elimu wa Jamhuri ya Czech,Mhe. Prof. Jaroslav Miller walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya sekta za afya za nchi zao.

Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Czech mwenye makazi yake Berlin, Ujerumani, Mhe. Dkt. Abdallah Possi akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Jakub Dvořáček walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya sekta za elimu za nchi zao.

 


 

WFP YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA SEKTA YA KILIMO NCHINI

Na Mwandishi wetu, Dar 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeahidi kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha kilimo nchini na kukifanya kuwa cha kisasa zaidi.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini mwa Afrika wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dkt. Menghestab Haile alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Haile amesema WFP inajivunia uhusiano mzuri na Tanzania na itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano huo kwa maslahi ya pande zote mbili.

“Leo tumejadili na kuona ni namna gani tunaweza kuwaunga mkono wakulima wa Tanzania ili waweze kupata faida zaidi kupitia kilimo ambapo faida hiyo itawasaidia kuyaboresha zaidi maisha yao,” amesema Dkt. Haile

“………… kwa kuwa kilimo ndiyo sekta pekee inayotoa fursa ya ajira kwa wingi duniani, tuna mkakati wa kuwawezesha vijana kujikita zaidi kwenye kilimo ili kupunguza tatizo la ajira,” amesema Dkt. Haile na kuongeza kuwa WFP itahakikisha Tanzania inakuwa kituo cha uzalishaji katika ukanda wa Kusini mwa Afrika kwa kuwa ina rasilimali za kutosha kuwekeza katika sekta ya Kilimo. 

Nae Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amemuahidi Mkurugenzi huyo wa WFP kuwa Serikali itatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha sekta ya kilimo nchini inaboreshwa zaidi.

“Nimewahakikishia WFP kuwa Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano katika kuhakikisha maboresho katika sekta ya kilimo yanafanyika na kuboresha maisha ya wakulima na kuwafanya vijana kujikita zaidi kwenye sekta hiyo muhimu,” amesema Balozi Mulamula.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na WFP katika kuboresha zaidi sekta ya kilimo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiongea na Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini mwa Afrika wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dkt. Menghestab Haile katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini mwa Afrika wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dkt. Menghestab Haile akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini mwa Afrika wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dkt. Menghestab Haile kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi wa Kanda ya Kusini mwa Afrika wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dkt. Menghestab Haile katika picha ya Pamoja Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Bibi. Sarah Gordon-Gibson wa kwanza kushoto, kulia mwa Balozi Mulamula ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Makocha Tembele anayefuatia ni Bw. Hlalanathi Fundzo kutoka WFP.  





Thursday, March 17, 2022

KAMATI YA KITAIFA YA KUZUIA MAUAJI YA KIMBARI YAJADILI MFUMO WA KUZUIA MIGOGORO NCHINI


 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. George Simbachawene (katikati) akifungua  kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari kinachofanyika jijini Dar es Salaam kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na kushoto ni bibi Cristine Musisi Mwakilishi mkazi wa UNDP nchini 
 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari kinachofanyika jijini Dar es Salaam katikati ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. George Simbachawene na kushoto ni bibi Cristine Musisi Mwakilishi mkazi wa UNDP nchini 


Mjwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari bibi Felistas Mushi akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Kamati hiyo kinachofanyika jijini Dar es Salaam

Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari katika picha ya pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. George Simbachawene (watatu kutoka kushoto waliokaa) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (watatu kutoka kulia waliokaa) baada ya kufunguliwa kwa kikao cha kamati yao kinachofanyika  Jijini Dar es Salaam kujadili uanzishwaji wa Mfumo wa kuzuia migogoro nchini


Na Mwandishi wetu, Dar es salaam

Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari imekutana Jijini Dar es Salaam kujadili uanzishwaji wa Mfumo wa kuzuia migogoro nchini ili kurahisisha shughuli za uratibu wa kamati hiyo.

Akifungua kikao cha kamati hiyo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. George Simbachawene amepongeza kuanzishwa kwa mfumo huo hapa nchini ambao utasaidia kutambua dalili za awali  katika matukio yanayoweza kusababisha kutokea mauaji ya kimbari.

“Naishukuru UNDP kwa kubuni wazo la kuanzishwa kwa mfumo huo, kwani kutambua dalili za awali za matukio yanayoweza kusababisha  kutokea kwa mauaji ya kimbari kutasaidia sana kuepusha kutokea kwa mauaji hayo siyo tu hapa nchini bali hata kwa nchi nyingine wanachama wa jumuiya yetu, ni wazo zuri na wadau wamelipokea vizuri,” amesema Mhe. Simbachawene.

Amesema Serikali inaendelea na taratibu za kuanzisha ofisi kwa ajili ya kuratibu mauaji ya kimbari hapa nchini kwa ajili ya kusaidia harakati za kuzuia kutokea kwa mauaji ya kimbari kupitia mfumo huo.

Kwa Upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameipongeza Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari ambayo imekuwa ikichukua hatua za kuwakutanisha wadau  mbalimbali katika jamii kama viongozi wa dini na jumuiya mbalimbali ili kutatua changamoto pale zinapotokea katika jamii nchini.

“Mimi kama mlezi wa kamati nimefarijika kuiona kamati hii ikitekeleza majukumu yake kwa ufanisi na siyo tu kuisaidia Tanzania bali hata nchi nyingine katika ukanda wa maziwa makuu,” amesema Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula amepongeza Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa kushirikiana na Serikali ya Uswisi kwa  kuona umuhimu wa Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari na hivyo kwa pamoja kuja na mpango wa kuanzishwa kwa kituo ambacho kitakuwa kinatoa taarifa za awali pale vinapokuwepo viashira vya matatizo au hata mauaji ya kimbari na kuongeza kuwa Serikali inaunga mkono jitihada hizo kwani zitaiwezesha kuzuia migogogo ambayo inaweza kusababisha kutokea mauaji  ya kimbari nchini.
  
Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari nchini iliundwa mwezi Februari, 2012 baada ya Tanzania kusaini na kuridhia Itifaki ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari iliyoridhiwa na Serikali ya Tanzania kupitia Mkataba wa nchi za Maziwa Makuu wa Usalama, Utulivu na Maendeleo.

Wednesday, March 16, 2022

WAZIRI MULAMULA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA BALOZI WA MALAWI

Na Waandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Baada ya kupokea nakala ya hati hizo Balozi Mulamula amemuahidi Balozi mteule ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ya kibalozi wakati wote atakaokuwepo nchini.

“Leo nimepokea nakala ya hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malawi na tumefarijika kwa Mhe. Rais Chakwera kumteua Balozi huyu mara baada ya Balozi wa awali kumaliza muda wake wa uwakilishi, hii ni ishara ya uhusiano wa karibu, undugu na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Malawi,” amesema Balozi Mulamula

Kwa upande wake Balozi Mteule wa Malawi Mhe. Andrew Kumwenda amesema kuwa Malawi na Tanzania siku zote zimekuwa na uhusiano mzuri wa kidiplomasia na jukumu langu hapa kama Balozi ni kuhakikisha uhusiano huu unazidi kuku ana kuimarika.

“Tanzania inatekeleza Diplomasia ya Uchumi na vivyo hivyo Malawi………kwa hiyo sisi wote tuna lengo moja, na nitahakikisha Tanzania na Malawi zinashirikiana kufanya biashara na uwekezaji kwa maslahi ya pande mbili,” Amesema Balozi Kumwenda.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akipokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiongea na Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula mara baada ya kuwasilisha nakala ya Hati za Utambulisho 

Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda yakiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Balozi Mteule wa Malawi nchini Mhe. Andrew Kumwenda katika picha ya pamoja na maafisa walioambatana nao   



Tuesday, March 15, 2022

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA KUSAIDIA KUWAREJESHA WANAFUNZI WALIOKUWA NCHINI UKRAINE

Na Waandishi Wetu, Dar 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) imeipongeza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa juhudi ilizozichukua hadi kufanikisha zoezi la kuwarejesha salama wanafunzi waliokuwa nchini Ukraine.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Vita Kawawa (Mb) Jijini Dar es Salaam wakati Kamati hiyo ilipotembelea Chuo cha Diplomasia (CFR).

Katika Kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mhe. Balozi Fatma Rajab.
“Nichukue nafasi hii kutoa pongezi nyingi kwa Wizara kwa jinsi mlivyoshughulikia suala zima la kuhakikisha wanafunzi wa Kitanzania walioko nchini Ukraine wanarejea salama nchini,” amesema Mhe. Kawawa.

‘’Mhe. Waziri tunawapa pongezi nyingi, kwa kazi  na hatua kubwa mlizochukua  na jinsi mlivyoshirikiana na wazazi wenye wanafunzi waliokuwa wanasom nchini Ukraine hasa ikizingatiwa kuwa wazazi hao waliwapeleka watoto wao binafsi bila ya kuishirikisha Serikali,’’ ameongeza Mhe. Kawawa.

Amesema kamati imeridhishwa na jinsi ambavyo Wizara ilivyosimama imara na kuwasaidia Watanzania wote waliokuwepo nchini Ukraine na kuhakikisha wanarejea nyumbani salama.

Mhe. Kawawa ametoa wito kwa Watanzania wanapokuwa nje ya nchi kujiandikisha katika Balozi za Tanzania ili kuwa rahisi kuwaratibu pale inapotokea athari yoyote kule wanapokuwepo.

Mhe. Kawawa amewapongeza vongozi wa wizara, mabalozi na watumishi wa wizara ambao kwa namna moja au nyingine wamefanikisha uondoaji wa watanzania waliokuwepo nchini Ukraine.
Akizungumza katika kikao hicho Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameihakikishia kamati hiyo kwamba Uongozi wake utaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha inasimamiwa ili ikamilike kwa wakati na kuendana na thamani halisi ya fedha iliyotolewa na Serikali.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa katika Chuo cha Diplomasia (CFR) Jijini Dar es Salaam

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula wakikagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya mihadhara ya Chuo cha Diplomasia (CFR) Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembelea Chuo Cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula. 

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembelea Chuo Cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Stella Ikupa akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembelea Chuo Cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)  katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula, Naibu Katibu Mkuu Balozi Fatma Rajab pamoja na viongozi wa Chuo  Cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam





 

BALOZI MULAMULA ATAJA MAFANIKIO WIZARA YA MAMBO YA NJE

Na Waandishi Wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ametaja maeneo 11 ambayo Wizara inajivunia katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita madarakani chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. 

Akiongea na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Balozi Mulamula amesema Wizara ya Mambo ya Nje katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita Wizara imetekeleza majukumu yake kwa mafanikio.

Balozi Mulamula ameyataja mafanikio hayo kuwa ni kusainiwa kwa makubaliano na mikataba ya ushirikiano katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa kufuatia ziara mbalimbali zilizofanywa na viongozi wa Kitaifa nje ya nchi na Wakuu wa nchi na Mashirika ya Kimataifa kutembelea nchini. 

“Ziara hizo pia zimewezesha upatikanaji wa misaada na mikopo ya masharti nafuu ambapo fedha kiasi cha Shilingi Trilioni 1.77 na Euro milioni 425 kutoka Kamisheni ya Umoja wa Ulaya zilipatikana, wakati huohuo Tanzania ilichaguliwa na nchi 192 wanachama wa Umoja wa Mataifa kuwa Makamu wa Rais wa Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambapo katika uchaguzi huo, Tanzania ilipita bila kupingwa, mara ya mwisho Tanzania kupata nafasi hiyo ilikuwa mwaka 1991,” amesema Balozi Mulamula.

Mafanikio mengine ni kufunguliwa kwa Balozi mpya mbili katika nchi za Austria na Indonesia na Konseli Kuu tatu katika miji ya Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Shanghai na Guangzhou nchini China, ikiwa ni pamoja na ukarabati wa majengo katika balozi za Tanzania.

Mafanikio mengine ni kuongezeka kwa wawekezaji kutoka nje ambapo wengi wameonesha dhamira ya kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali. 

Balozi Mulamula amesema Lugha ya Kiswahili kwa mara ya kwanza kiswahili kimetambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kuwekewa siku maalum ya kuadhimishwa duniani ambayo ni tarehe 7 Julai kila mwaka. Niwakumbushe kuwa, Kiswahili ni lugha ya kwanza ya kiafrika kupewa hadhi hiyo na UNESCO," Amesisitiza Balozi Mulamula.

Mafaniko mengine yaliyoainishwa na Mhe. Waziri wakati wa mkutano huo ni pamoja na kuondolewa kwa vikwazo 56 kati ya 64 vya kibiashara kufuatia maagizo ya Marais wa Kenya na Tanzania. Aidha, vikwazo vingine vinane viliondolewa na Mawaziri wa Biashara wa nchi hizi mbili walipokutana Zanzibar tarehe 13 Machi 2022.

Kadhalika, Waziri Mulamula amesema Wizara yake itaendelea kutekeleza Sera ya Mambo ya Nje hususan kwenye masuala ya kukuza uchumi wa nchi kwa kuhamasisha uwekezaji kutoka nje, biashara na utalii. 

Balozi Mulamula amehitimisha na Suala la Watanzania waliokuwa wamekwama nchini Ukraine ambapo amesema serikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha raia wake wanakuwa salama pamoja na changamoto hizo. 

“Napenda kuwafahamisha kuwa, zoezi la kuwaondoa Watanzania wote waliokuwepo nchini humo wakiwemo Wanafunzi limekamilika ambapo hadi sasa takribani Watanzania 300 wamefanikiwa kuondoka na kuelekea nchi jirani na baadhi yao wamerejea hapa nchini”, amesema Balozi Mulamula.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akiwasilisha taarifa ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akisikiliza moja kati ya maswali yaliyoulizwa na baadhi ya waandishi wa habari (hawapo pichani) alipowasilisha taarifa ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiongea na waandishi wa habari  alipokuwa akiwasilisha taarifa ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita  




Monday, March 14, 2022

BALOZI WA MAREKANI APONGEZA UENDESHAJI MICHAKATO YA KISIASA NCHINI

 

Na Waandishi wetu, Dar


Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Donald Wright amepongeza uendeshaji wa michakato ya kisiasa inavyoendeshwa nchini Tanzania. 

Balozi Wright ameyasema hayo wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Balozi Wright amesema anaridhishwa na jinsi hali ya kisiasa ilivyo hapa nchini na kuongeza kuwa anaunga mkono michakato ya kisiasa inavyoendeshwa nchini na kuelezea kuridhishwa kwake na hali hiyo. 
 
Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani kwa maslahi ya pande zote mbili. 

Naye Waziri Mulamula amemuahidi Dkt. Wright kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake wakati wote hapa nchini.

Katika tukio jingine, Waziri Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Mhe. Elisabeth Jacobsen na kujadili masuala ya ushirikiano katika masuala ya amani na usalama, jinsia na uwezeshaji wa wanawake.

Pia, Waziri Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Afisa kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bibi. Jacqueline Machangu-Motcho na kujadili masuala ya ushirikiano baina ya mfuko huo na Tanzania.

Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Donald Wright akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Donald Wright  

Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Donald Wright kikiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Norway nchini Mhe. Elisabeth Jacobsen katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza Afisa kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bibi. Jacqueline Machangu-Motcho katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



BALOZI SOKOINE AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA SADC MJINI LILONGWE, MALAWI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph E. Sokoine akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha kawaida cha Baraza la Mawaziri wa SADC kinachofanyika Lilongwe nchini Malawi. Nyuma ya Balozi Sokoine kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Exavier Daudi anayefuata ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Agnes Kayola pamoja na Afisa dawati.



Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kikiendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Bingu wa Mutharika Lilongwe, Malawi

 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC. Kushoto kwa Balozi Sokoine ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi Bw. Exavier Daudi na kulia kwa Balozi Sokoine ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Shaaban
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine ukijadili mwenendo wa kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kuhusu maslahi ya Tanzania, Lilongwe, Malawi

Friday, March 11, 2022

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI SAUDI ARABIA


 

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini (kushoto) akiwa amekaa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Nyumbani kwake jijini Riyadh wakati alipomualika Mhe. Waziri kuzungumza na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati Waziri Mulamula alipokuwa na ziara ya kikazi nchini humo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati alipokutana nao nyumbani kwa Mhe. Balozi Mwadini jijini Riyadh
Mwakilishi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia Bi Amina akisoma risala kwa Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh 
Bi Amina akiwasilisha nakala ya risala aliyoisoma kwa Mhe. Waziri Mulamula alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh

Mwakilishi wa Watanzania wanawake wanaoishi nchini Saudi Arabia akimkabidhi zawadi Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia Dkt. Msechu akimkabidhi zawadi Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh  

 

Balozi Mulamula mwenye (ushungi wa bluu) akiwa na Waziri wa Maliasili na Utaalii Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kushoto) Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) pamoja na viongozi wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati walipokutana na Mawaziri hao nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini jijini Riyadh.

 


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia na kuwataka kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania nchini humo.

Balozi Mulamula amekutana na Watanzania hao jijini Riyadh katika kikao kilichofanyika nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini.

Akizungumza na Watanzania hao Balozi Mulamula amesisitiza juu ya umuhimu wa Watanzania hao kuishi kwa kufuata sheria na kanuni za nchi hiyo kwani kufanya hivyo kutaendelea kulinda taswira nzuri ya nchi yao.

Balozi Mulamula pia amewahahakishia watanzania hao juu ya nia ya Serikali ya kufanyia kazi mawazo na maoni yao ili kuwa kuwa na amani.

‘’Niwahakikishieni ndugu zetu mlioko huku, serikali yenu ni sikivu inathamini na kujali maoni mnayoyatoa na inayafanyia kazi, na muda si mrefu mtaona tulipofikia,” alisema Balozi Mulamula.

Awali katika risala yao kwa mhe. Waziri Watanzania hao walielezea changamoto na mafanikio yaliyopatikana kupitia umoja wao na kuiomba serikali kufanyia kazi changamoto wanazozipata hasa wakati wa kuondoka nyumbani.

Waziri Mulamula yuko nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia Mwana Mfalme, Mtukufu Faisal bin Farhan Al Saud, alioutoa mwezi Machi 2021 alipotembelea Tanzania.