Friday, March 11, 2022

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI SAUDI ARABIA


 

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini (kushoto) akiwa amekaa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Nyumbani kwake jijini Riyadh wakati alipomualika Mhe. Waziri kuzungumza na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati Waziri Mulamula alipokuwa na ziara ya kikazi nchini humo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati alipokutana nao nyumbani kwa Mhe. Balozi Mwadini jijini Riyadh
Mwakilishi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia Bi Amina akisoma risala kwa Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh 
Bi Amina akiwasilisha nakala ya risala aliyoisoma kwa Mhe. Waziri Mulamula alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh

Mwakilishi wa Watanzania wanawake wanaoishi nchini Saudi Arabia akimkabidhi zawadi Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia Dkt. Msechu akimkabidhi zawadi Balozi Mulamula wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia  nyumbani kwa Balozi wa Tanzania jijini Riyadh  

 

Balozi Mulamula mwenye (ushungi wa bluu) akiwa na Waziri wa Maliasili na Utaalii Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kushoto) Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) pamoja na viongozi wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia wakati walipokutana na Mawaziri hao nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini jijini Riyadh.

 


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia na kuwataka kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania nchini humo.

Balozi Mulamula amekutana na Watanzania hao jijini Riyadh katika kikao kilichofanyika nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini.

Akizungumza na Watanzania hao Balozi Mulamula amesisitiza juu ya umuhimu wa Watanzania hao kuishi kwa kufuata sheria na kanuni za nchi hiyo kwani kufanya hivyo kutaendelea kulinda taswira nzuri ya nchi yao.

Balozi Mulamula pia amewahahakishia watanzania hao juu ya nia ya Serikali ya kufanyia kazi mawazo na maoni yao ili kuwa kuwa na amani.

‘’Niwahakikishieni ndugu zetu mlioko huku, serikali yenu ni sikivu inathamini na kujali maoni mnayoyatoa na inayafanyia kazi, na muda si mrefu mtaona tulipofikia,” alisema Balozi Mulamula.

Awali katika risala yao kwa mhe. Waziri Watanzania hao walielezea changamoto na mafanikio yaliyopatikana kupitia umoja wao na kuiomba serikali kufanyia kazi changamoto wanazozipata hasa wakati wa kuondoka nyumbani.

Waziri Mulamula yuko nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia Mwana Mfalme, Mtukufu Faisal bin Farhan Al Saud, alioutoa mwezi Machi 2021 alipotembelea Tanzania.

 

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.