Friday, March 4, 2022

WIZARA YAKABIDHI OFISI KWA CHAMA CHA MABALOZI WASTAAFU NCHINI



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kushoto) akizungumza wakati wa kukabidhi Ofisi kwa Chama cha Mabalozi Wastaafu nchni.
Mwenyekiti wa Chama cha Mabalozi Wastaafu nchini Balozi Celestine Christopher Liundi (kulia) akishukuru wakati wa hafla ya kukabiddhiwa Ofisi kwa Chma hicho huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kushoto) wakimsikiliza 
Mwenyekiti wa Chama cha Mabalozi Wastaafu nchini Balozi Celestine Christopher Liundi (kulia) akizungumza wakati wa hafla ya kukabiddhiwa Ofisi kwa Chma hicho huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kushoto) wakimsikiliza
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kushoto) wakimsikiliza katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Mabalozi Wastaafu nchini wakati wa hafla ya kukabiddhiwa Ofisi kwa Chama hicho zilizofanyika Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Mabalozi Wastaafu nchni na baadhi ya viongozi wa Wizara wakati wa hafla ya kukabiddhiwa Ofisi kwa Chama hicho zilizofanyika Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam. 



 

Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki umekabidhi ofisi kwa chama cha mabalozi Wastaafu nchini (ARTA).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekabidhi ofisi hizo zilizopo katika jengo la Wizara jijini Dar es salaam kwa niaba ya Wizara na kuhudhuriwa na baadhi ya viongozi wa wizara na watumishi .

Akikabidhi ofisi hizo Balozi Mulamula amesema ofisi hiyo iliyoko katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam itatatumiwa na mabalozi wastaafu hapa nchini ili kuwawezesha mabalozi hao kuendelea kutoa mchango wao katika ujenzi wa Taifa hususani katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi.

Akizungumza kwa niaba ya chama cha mabalozi wastaafu Mwenyekiti wa chama hicho Balozi Celestine Liundi amesema chama hicho kwa sasa kina wanachama hai 57 ambao bado wanaweza kuisaidia nchi katika nyanja ya uhusiano wa kimataifa. 

Balozi Liundi ameushukuru uongozi wa Wizara kwa kitendo cha kuwapatia ofisi ndani ya jengo la Wizara na kuongeza kuwa kitendo hicho kimewatia moyo wa kuendelea kutoa ushauri,mapendekezo na michango ya mawazo katika kuendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Mataifa mengine.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.