Tuesday, March 8, 2022

Tanzania Yashiriki Maadhimisho ya Miaka 25 ya IORA

Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika  Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amewasilisha kwa njia ya mtandao salamu za pongezi ya Miaka 25 ya Jumuiya ya Nchi Wanachama wa Mwambao wa Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim Assocaition-IORA) yaliyofanyika jijini Mapou, Mauritius tarehe 7 Machi 2022.

Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki imewakilishwa na Balozi Agnes Richard Kayola, Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda aliyeambatana na Dkt. Mnata Resani,  Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Utamaduni kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Katika Maadhimisho hayo, nchi wanachama zimepata fursa ya kutangaza Utamaduni wao kwa kupitia vyakula, nyimbo na ngoma za asili. Tanzania iliandaa chai na kahawa ya hapa nchini na Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) kilitumbwiza kwenye maadhimisho hayo.


Watu mbalimbali wakichukua vyakula vya Kitanzania vilivyoandaliwa kwa ajili ya kuadhimisha miaka 25 ya Jumuiya ya Nchi Wanachama wa Mwambao wa Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim Assocaition-IORA) yaliyofanyika jijini Mapou, Mauritius tarehe 7 Machi 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Mauritius, Mhe. Alan Ganoo
 akitoa neno wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 25 ya umuiya ya Nchi Wanachama wa Mwambao wa Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim Assocaition-IORA) yaliyofanyika jijini Mapou, Mauritius tarehe 7 Machi 2022.

Mkurugenzi wa Idara ya Ushrikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola akiwa na wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Mauritius.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.