Wednesday, March 2, 2022

TANZANIA IRELAND KUENDELEZA USHIRIKIANO

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwa Balozi wa Jamhuri ya Ireland nchini.


 

Balozi wa Ireland nchini Mhe. Mary O’Neil akizungumza wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki , Balozi Swahiba Mndeme (kulia) wakimsikiliza Balozi wa Ireland nchini Mhe. Mary O’Neil  akizungumza wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Comoro na  Mkuu wa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini Mhe.Ahmada El Badaoui Mohamed Fakih wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwa Balozi wa Ireland jijini Dar es Salaam.


Balozi wa Kenya nchini  Mhe. Dan Kazungu (katikati) akijadili jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) walipokutana nyumbani kwa Balozi wa Ireland nchini Mhe. Mary O’Neil kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick ambayo huadhimishwa nchini humo tarehe 17 Machi ya kila mwaka .


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Canada nchini Mhe. Pamela O’Donnell  wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwa Balozi wa Jamhuri ya Ireland nchini (kulia) akiwaangalia.


Baadhi  ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania walioshiriki sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick zilizofanyika nyumbani kwa Balozi wa Jamhuri ya Ireland jijini Dar es Salaam.



 

Tanzania na Ireland zimeahidi kuendeleza uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo kwa manuufaa ya pande zote mbili

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametoa ahadi hiyo aliposhiriki katika maadhimisho ya Siku ya Mtakatifu Patrick ambayo huadhimishwa na Jamhuri ya Ireland tarehe 17 ya kila mwaka.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku hiyo Waziri wa Mulamula ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Ireland kwa kuendelea kuwa mdau mkubwa wa maendeleo wa Tanzania hasa katika Nyanja za kusaidia kaya masikini, elimu na kuwajengea uwezo wanawake na watoto wa kike nchini.

Amesema Serikali inathamini mchango wa Ireland kwa Tanzania na kusisitiza kuwa itaendeleza uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo ili kufikia maendeleo ya kweli kwa pamoja.

Naye Balozi wa Ireland nchini Mhe. Mary O’Neil ameahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada za kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Ireland na kuahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa faida ya wananchi wa nchi zote.

Maadhimisho ya siku hiyo yamezinduliwa rasmi leo Tarehe 02 Machi 2022 jijini Dar es Salaam katika makazi ya Balozi wa Ireland nchini na kuhudhuriwa na Mabalozi na Wawakilishi wa Taasisi za Kimataifa wanaoziwakilisha nchi na Mashirika yao hapa nchini.

Siku ya Mtakatifu Patrick huadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 Machi nchini Ireland kuadhimisha kuwasili kwa ukristo nchini humo na kusherehekea urithi wa utamaduni wa watu wa Ireland kwa ujumla.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.