Monday, March 14, 2022

BALOZI SOKOINE AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA SADC MJINI LILONGWE, MALAWI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph E. Sokoine akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha kawaida cha Baraza la Mawaziri wa SADC kinachofanyika Lilongwe nchini Malawi. Nyuma ya Balozi Sokoine kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Exavier Daudi anayefuata ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Agnes Kayola pamoja na Afisa dawati.



Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kikiendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Bingu wa Mutharika Lilongwe, Malawi

 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC. Kushoto kwa Balozi Sokoine ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi Bw. Exavier Daudi na kulia kwa Balozi Sokoine ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Shaaban
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine ukijadili mwenendo wa kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kuhusu maslahi ya Tanzania, Lilongwe, Malawi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.