Tuesday, December 27, 2016

Wizara ya Mambo ya Nje yafanya kikao cha cha pamoja cha watumishi kujadili masuala ya kiutendaji

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akizungumza na watumishi wa Wizara hawapo pichani, kwenye kikao cha pamoja kilichofanyika leo katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu, Bw. Hamid Mbegu.

Sehemu ya Wakurugenzi wakifuatilia kikao, kutoka kushoto Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Baraka Luvanda.
Sehemu nyingine ya Wakurugenzi, katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Bw. Stephen Mbundi, Kulia ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara, Bi. Mindi Kasig.
Watumishi wakifuatilia kikao.

Sehemu ya watumishi wakifuatilia kikao.


Sehemu nyingine ya watumishi wakifuatilia kikao.

===============================================
Wakati huo huo uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki umetumia fursa hiyo kutoa zawadi kwa Idara na vitengo vilivyofanya vizuri kwa kipindi cha mwaka 2016.

Balozi Mbelwa Kairuki akionyesha zawadi mara baada ya kukabidhiwa na Waziri Mahiga. 

Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Bw. Mbundi akipokea zawadi ya Idara ya zilizofanya vizuri. Pamoja na Idara hizo Idara nyingine zilizoingia tano bora ni pamoja na Idara ya Amerika na Ulaya, Idara ya Afrika na Kitengo cha Fedha na Uhasibu.

Mfano wa Zawadi iliyokabidhiwa kwa Idara na vitengo vilivyoshinda na kuingia katika tano bora.

Kikao kikiendelea.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.