Wednesday, May 10, 2017

Rais wa Afrika Kusini awasili nchini kwa Ziara ya Kiserikali


Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma akiwa ameambatana na mkewe Mama Getrude SizakeleZuma wakishuka  kwenye ndege baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya siku mbili inayotarajiwa kumalizika tarehe 11 Mei, 2017. 
Juu na chini Mhe. Rais Jacob Zuma na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Mhe.  Jacob Zuma Rais wa Afrika Kusini akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi mara baada ya kuwasili  leo tarehe 10 Mei 2017.
Mhe.  Rais Jacob Zuma akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Suleiman Saleh Kulia nia Mkuu wa Itifaki na Mkurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin. 
Mhe. Rais Zuma akisalimiana na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dar es salaam waliofika Uwanaja wa Ndege kwenye mapokezi rasmi yaliyoongozwa na Mhe. Dk. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.