Sunday, May 28, 2017

Waziri Mahiga aongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga leo ameongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara. Hotuba hiyo inatarajiwa kuwasilishwa Bungeni hapo kesho tarehe 29 Mei, 2017.

Kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma katika ukumbi mikutano wa jengo la Hazina pia kimehudhuriwa  na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Susan Kolimba, Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima Wakurugenzi ,Wakuu wa Vitengo na baadhi ya Maafisa wa Wizara.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Naibu Mhe. Dkt. Susan Kolimba wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu Balozi Dkt.Aziz Mlima.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na  Naibu Waziri Mhe.Dkt.Susan Kolimba wakishirikishana jambo wakati wa Kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara.

Mhasibu Mkuu wa Wizara Bw. Paul Kabale akichangia jambo wakati wa kikao

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akichangia jambo wakati wa kikao

Kaimu Mkurugenzi  wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule (kulia) akichangia jambo wakati wa kikao

Wajumbe wakiwa katika kikao

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.