Friday, May 12, 2017

Wizara ya Mambo ya Nje yapokea magari ya msaada







Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) (katikati), akipokea funguo za Magari aina ya Toyota Land Cruiser  kutoka kwa  Balozi wa Kuwait hapa nchini, Mhe. Jasem Al-Najem. Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam leo. Waziri Mahiga alisema kuwa msaada huo umetolewa na Serikali ya Kuwait kwa ajili ya kusaidia masuala ya usafiri katika kipindi hiki cha mpito ambapo Serikali inahamia Dodoma. 
Waziri Mahiga akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Serikali na Wizara yake kwa ujumla mara baada ya kupokea msaada huo. 
Balozi Al-Najem naye akizungumza na kuishukuru Tanzania kwa ushirikiano anaoumpata kwenye utendaji kazi wake hapa nchini. Alisema Serikali yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwemo huduma za kijamii.
Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wa pili kutoka kulia ni Afisa Ubalozi wa Kuwait haapa nchini.
Sehemu nyingine ya viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutoka kulia ni Mhasibu Mkuu, Bw. Paul Kabale; Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi (wa pili kutoka kulia), Bw. Mapesi Manyama, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika,  Bw. Suleiman Saleh; Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga, kutoka kushoto ni Maafisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kutoka kushoto ni  na wa pili kutoka kushoto ni Bw. Hangi Mgaka
Waziri akiendelea kuongea huku Watumishi wa Wizara yake wakimsikiliza kwa makini.

Picha ya pamoja mara baada ya shughuli kumalizika.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.