Tuesday, July 28, 2020

HAFLA YA MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS WA AWAMU YA TATU WA TANZANIA- HAYATI BENJAMIN MKAPA



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali wilbert Ibuge(wa kwanza kushoto), akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli katika Viwanja vya Uhuru kwa ajili ya kuongonza hafla ya Kitaifa ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania Mhe. Hayati Benjamin William Mkapa, aliyefariki dunia tarehe 24 Julai 2020, Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi(aliyesimama mwisho kulia), akisoma wasifu wa Mhe, Hayati Mkapa.

  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Jenerali Alain                   Guillaume Bunyoni, akitoa salam za rambirambi kutoka Nchi ya        Burundi, Jenerali Bunyoni pia ameambatana na Spika wa Bunge la    Nchi hiyo pamoja na viongozi wengine kutoka nchini humo.

Kiongozi(Dean) wa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini, Balozi wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed Fakih, akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Mabalozi wenzake. 

   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe          Magufuli akihutubia viongozi na wananchi waliohudhuria hafla ya    Kitaifa ya kumuaga Rais wa awamu ya tatu, Mhe. Hayati Mkapa.   
  akiongea katika hotuba yake alisisitiza Watanzania kuenzi mambo      mengi mazuri aliyoyaacha Hayati Mkapa, Mhe. Magufuli alisema      "Ninamshukuru Mungu kwa zawadi ya Maisha ya Mkapa".

 Baadhi ya Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania Nje ya nchi  pamoja  na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania (waliosimama mistari mitatu ya mwisho) wakiwa katika hafla hiyo

   Baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini
   ( mistari miwili ya mwisho) wakifuatilia shughuli hiyo


       Mawaziri waliohudhuria wakifuatilia shughuli hiyo


   Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw. Libarat                Mfumukeko( wa pili kulia), akiongozwa na Afisa Itifaki Bw. Ishengoma kuingia uwanjani kushiriki shughuli hiyo

    Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakitoa heshima     za mwisho kwa mwili wa Hayati Mkapa

         Mabalozi wakiendelea kutoa heshima za mwisho


     Mabalozi wakiendelea kutoa heshima za mwisho

  Mhe. Kabudi akimuaga Mhe. Magufuli alipokuwa akitoka uwanjani

   Mhe. Kabudi akiagana na Waziri Mkuu wa Burundi, Mhe. Bunyoni


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika                  Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro(Katikati),                              akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe.                  Hamad Masauni(Kulia), baada ya hafla hiyo kumalizika

    








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.