Monday, July 6, 2020

KATIBU MKUU BALOZI BRIGEDIA JENERALI IBUGE ATEMBELEA BANDA LA WIZARA SABASABA


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, ametembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Wizara Balozi Ibuge amewataka Watanzania kuendelea kuchapa kazi zaidi ili kuyaona matunda ya nchi kuwa katika kundi la uchumi wa kati.

''Sasa nchi yetu imeingia katika uchumi wa kati ambao unamaanisha kila mtu aendelee kupiga juhudi zaidi ya pale alivyokuwa anafanya ili tuendelee kupaa kuliko hivi ambavyo tumefikia sasa'' amesema Balozi Ibuge.

Amesema Tanzania sasa ina Balozi 43 na Balozi ndogo tatu na ni mwenyeji wa Balozi 63 na Mashirika ya Kimataifa 30 ikiwa ni namna ya kuipeleka Tanzania katika anga za kimataifa tukionyesha mafanikio vivutio vyetu na vitu vingine vyote tunavyovifanya ili kujiletea maendeleo huku tukiimarisha mahusiano ya kimataifa.

Akiwa katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Balozi Ibuge ametembelea banda la Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) na makampuni matatu ya Kigeni yanayoshiriki maonesho hayo.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akizungumza na watumishi alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akiangalia jarida linaloelezea utekelezaji wa dipolomasia ya uchumi linalochapishwa na Wizara alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, katika picha ya pamoja na watumishi walioko kwenye banda la Wizara katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba)

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akijadili jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dkt. Ave Maria Semakafu walipotembelea moja ya banda kwenye maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dkt. Ave Maria Semakafu wakimsikiliza mfanyabiashara kutoka Siria anayeshiriki maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) katika maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) 2020 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.