Tuesday, October 6, 2020

RAIS DKT MAGUFULI AMUANDIKIA BARUA YA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIONGOZI MPYA WA KUWAIT

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemwandikia barua ya salamu za rambirambi Kiongozi mpya (Amir) wa Kuwait, Mtukufu Sheikh Nawaf Al-Ahmad Al-Sabah kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait hapa nchini amemkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait.

Prof. Kabudi amesema Tanzania na Kuwait zina mahusiano mazuri sana na muda mrefu katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo akitolea mfano wa mfuko wa Kuwait ambao umekuwa wa msaada mkubwa katika kwa Tanzania ambao umekuwa ukisaidia katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali hapa nchini ikiwemo barabara.

Ameongeza kuwa msiba wa Kiongozi huyo wa Kuwait ni msiba wa Watanzania wote kwa kuwa kwa muda wote ambao Hayati Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah amekuwa Kiongozi wa Taifa hilo amekuwa karibu sana na Tanzania.


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait nchini, kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akimkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait


 


Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John mara baada ya kumaliza kusaini kitabu cha maombolezo 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.