Wednesday, October 7, 2020

RAIS MHE.DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMPOKEA MGENI WAKE RAIS WA MALAWI DKT. LAZARUS CHAKWERA JIJINI DAR ES SALAAM

 


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi akiongea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati walipokuwa wakimsubiri Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam. Kushoto mwa Balozi Kijazi ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akikagua Gwaride la Heshma lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam 



Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) kutoka Tanzania na Malawi mara baada ya mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari kutoka Tanzania na Malawi (hawapo pichani) katika mkutano na Waandishi wa Habari mara baada ya mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera


Waziri wa Mabo ya Ndani Mhe. George Simbachawene mwenye (suti ya blue) pamoja na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (kushoto) wakiwa pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali wakifuatilia mkutano wa pamoja wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Chakwera wakati walipokuwa wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.