Tuesday, February 16, 2021

TANZANIA MBIONI KUSAINI MKATABA WA ENEO HURU LA BIASHARA YA UTATU COMESA-EAC-SADC


Tanzania imeshiriki katika Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliofanyika kwa njia ya video. Katika mkutano huo moja ya agenda ilikuwa nchi Wanachama kutoa taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa katika kusaini na kuridhia mkataba wa kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara ya Utatu ya COMESA-EAC-SADC. Katika mkutano huo Tanzania kupitia Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Dkt. Leonard Chamuriho imeeleza kuwa ipo katika hatua za kusaini na kuridhia mkataba huo. 

Mkutano huo ulioitishwa kwa dharura pia ulilenga kupitia na kujadili rasimu ya mwongozo wa utatu wa usimamizi na ufuatiliaji wa uvukaji salama wa watu na bidhaa mipakani katika kipindi hiki cha Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19). Jumuiya za COMESA, EAC na SADC baada ya kugundua kuwa nchi mbalimbali ziliaandaa miongozo ya kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19 bila kuathiri uchumi na biashara iliamua kuratibu maandalizi ya miongozo ya kikanda ili kuondokana na changamoto za biashara baina ya nchi wanachama. Nchi wanachama zimekubaliana kuwa mkutano uitishwe tena baada ya wiki mbili ili kujadili agaenda hii na kufikia maamuzi ya pamoja.

Katika mkutano huo kwa upande wa Tanzania ulihudhuriwa na Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Geofrey Pinda Watendaji na Maafisa mbalimbali wa Serikali


Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Dkt. Leonard Chamuriho, Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Geofrey Pinda wakifuatilia Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliokuwa ukiendelea kwa njia ya video


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akifuatilia Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliokuwa ukiendelea kwa njia ya video
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Dkt. Leonard Chamuriho akichangia jambo katika Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliofanyika kwa njia ya video

Badhi ya Watumishi wa Serikali waliohudhuria Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliokuwa ukiendelea kwa njia ya video wakifualia mjadala uliokuwa ukiendelea
Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Dkt. Leonard Chamuriho, Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Geofrey Pinda wakifuatilia Mkutano wa Pili wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Utatu uliokuwa ukiendelea kwa njia ya video

Mkutano ukiendelea

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.