Wednesday, February 3, 2021

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa 38 wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia ya video. Anayeonekana katika Screen pichani ni Waziri wa Ushirikiano na Uhusiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. Dkt. Naledi Pandor anayeongoza mkutano huo


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia Mkutano wa 38 wa Baraza la Mawaziri Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia ya video

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi na ujumbe wa Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa 38 wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia ya video.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia ufunguzi wa Mkutano huo unaofanyika kwa njia ya video. 


Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia video (video conference) umeanza.Mkutano huo umefunguliwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la Umoja huo na Waziri wa Ushirikiano na Uhusiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini Mhe. Dkt. Naledi Pandor

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi ameongoza ujumbe wa Tanzania kutokea katikaa mji wa Serikali Mtumba ulioko Makao Makuu ya nchi jijini Dodoma.

Mkutano huo wa kawaida wa siku mbili unaongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. Dr. Naledi Pandor Waziri wa Ushirikiano na Uhusiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini pamoja na mambo mengine utaandaa rasimu ya agenda za Mkutano wa 34 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika utakaofanyika tarehe 6 na 7 Februari, 2021 kwa njia video  

Mkutano huo unajadili na kupitisha mapendekezo ya taarifa ya Mkutano wa 41 wa Kamati ya Kudumu ya Uwakilishi (Permanent Representatives Committee –PRC),taarifa ya hali ya ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu (COVID-19) Barani Afrika na taarifa ya Mkutano wa Pamoja wa Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Tathimini na Kamati ya Mawaziri 15 wa Fedha.

Mkutano pia utafanya uchaguzi na Uteuzi wa Wajumbe Sita (6) wa Bodi ya Ushauri ya Masuala ya Rushwa ya Afrika, Makamishna wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Majaji wanne (4) wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu.

 

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.