Wednesday, January 12, 2022

BALOZI FATMA ASHIRIKI KIKAO KAMATI YA FEDHA SADC

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab ameshiriki katika kikao cha Kamati ya Fedha ya SADC kilichofanyika Jijini Lilongwe, nchini Malawi. 

Kikao hicho kimetanguliwa na Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji ulioanza tarehe 11 Januari 2021 Lilongwe, Malawi.

Katika Mkutano wa Dharuar wa Wakuu wa Nchi na Serikali, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika kikao cha Kamati ya Fedha ya SADC kilichofanyika Jijini Lilongwe, nchini Malawi

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika kikao cha Kamati ya Fedha ya SADC



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.