Saturday, January 15, 2022

BALOZI HEMEDI MGAZA AKUTANA NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI KUWAIT

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemedi Mgaza (kulia)amefanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Said Shaibu Mussa alipokuja kuaga uongozi wa Wizara tarehe 14 Januari 2022 jijini Dodoma.

Viongozi hao walijadili hali halisi ya utekelezaji wa majukumu ndani ya Idara ya Mashariki ya Kati na kuweka mikakati madhubuti ya usimamizi wa majukumu katika dawati la Kuwait linaloratibiwa na idara hiyo.
Kwa pamoja wameazimia kufanya kazi kwa ushirikiano, kusimamia miradi ya ushirikiano inayoendela katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu inayofadhiliwa na Mfumo wa Kuwait hususani miradi ya kilimo, maji, ujenzi wa miundombinu, afya, elimu na ajira za kitaalamu.

Balozi Mgaza akimkaribisha Mhe. Said Shaibu Mussa katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.