Tuesday, January 11, 2022

DKT. MPANGO AMWAKILISHA RAIS SAMIA MKUTANO WA DHARURA MALAWI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura Wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji ulioanza leo tarehe 11 Januari 2022 Lilongwe, Malawi.

Awali akifungua Mkutano huo, Rais wa Afrika Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa TROIKA Mhe. Cyril Ramaphosa amesisitiza umuhimu wa nchi wanachama kuiunga mkono Jamhuri ya Msumbiji katika Mapambano yake dhidi ya mashambulizi ya kigaidi yanayoikabili nchi hiyo hasa Katila jimbo la Cabo Delgado.

Aidha, Mhe. Ramaphosa ameongeza kuwa kuna umuhimu kwa SADC kushirikiana katika kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya jumuiya hiyo.

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo wa dharura umeongozwa na Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Edward Komba pamoja na Maafisa wengine waandamizi wa Serikali.

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango akifuatilia Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji. Mkutano umefanyika Lilongwe Malawi. Kulia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango akiongoza ujumbe wa Tanzania katika ukumbi wa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji leo Lilongwe, Malawi

Baadhi ya Ujumbe wa Tanzania, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajab pamoja na Maafisa Waandamizi wa Serikali

Rais wa Jamhuri ya Malawi na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Mhe. Lazarus Chakwera akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango, pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Bishara za Kimataifa wa Zimbabwe Balozi Frederick Shawa kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji. Mkutano umefanyika Lilongwe, Malawi.

Rais wa Jamhuri ya Malawi na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Mhe. Lazarus Chakwera akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango muda mfupi kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji, Lilongwe, Malawi
Wakuu wa Nchi na Wawakilishi wa Wakuu wa Nchi walioshiriki katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano katika Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya SADC, Jamhuri ya Msumbiji na Nchi zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyoko nchini Msumbiji wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa kwa Mkutano huo leo Lilongwe, Malawi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.