Tuesday, May 21, 2019

VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE AU COMMISSION


Dodoma, 21st May 2019

PRESS RELEASE

Job Announcement at the African Union Commission

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the Commission of African Union inviting qualified Tanzanians to apply for the posts available at the Commission.

The vacant positions currently available in the commission are as follows:-
Position
Department
Location
Deadline
DIRECTOR OF TRADE AND INDUSTRY
Department of Trade and Industry
Ethiopia
3/6/2019
DIRECTOR OF PEACE AND SECURITY
Peace and Security Department
Ethiopia
10/6/2019
HEAD CRISIS MANAGEMENT AND POST-CONFLICT RECONSTRUCTION DIVISION (CMPCRD)
Peace and Security Department
Ethiopia
10/6/2019

Details of the positions are available through the AUC E-recruitment Website http://aucareers.org/.


Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation.


Monday, May 20, 2019

Tanzania na Uholanzi zazindua Mradi wa Kukua na Kuku



Dodoma, 20 Mei 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania na Uholanzi zazindua Mradi wa Kukua na Kuku

Ubalozi wa Tanzania nchini Uholanzi kwa kushirikiana na Baraza la Biashara la Uholanzi na Africa (Netherlands – Africa Business Council - NABC) hivi karibuni waliongoza ujumbe wa Makampuni 7 kutoka Uholanzi yaliyobobea katika Sekta ya Ufugaji wa Kuku kwenda Mkoani Kilimanjaro kuzindua Mradi maalum wa ufugaji utakaoendeshwa na Makampuni hayo nchini Tanzania maarufu kama “Kukua Na Kuku (Growing with Chicken) Impact Cluster”.
      Mradi wa “Kukua Na Kuku” ni matokeo ya makubaliano ya kuanzisha ubia kati ya Tanzania na Uholanzi yanayolenga kuboresha Sekta ya Ufugaji Kuku nchini Tanzania na kuifanya kuwa endelevu kwa kutumia teknolojia ya kisasa kutoka Uholanzi. Makampuni hayo yatatoa mafunzo kwa lengo la kuwajengea uwezo wafugaji wazawa kwa kuboresha usimamizi wa kilimo cha ufugaji, afya ya wanyama, upatikanaji wa chakula (lishe) bora kwa ajili ya mifugo, vifaa muhimu vya kufugia, na hata utafutaji masoko.
Uzinduzi huo ulifanyika kwenye Chuo cha Kilimo na Ufugaji wa Mifugo Kilacha, Mkoani Kilimanjaro kwa kusaini Makubaliano ya Ushirikiano, na ukawa ndio mwanzo wa ushirikiano wa miaka 3 kati ya makampuni hayo 7, Serikali ya Uholanzi na wadau wazawa wa Tanzania. Chuo cha Kilimo na Ufugaji wa Mifugo cha Kilacha kinasimamiwa na Kituo cha Uzalishaji na Mafunzo kinamilikiwa na Kanisa Katoliki Mkoani humo.
Mgeni rasmi wakati wa sherehe za uzinduzi huo alikuwa Mhe. Anna Mgwira, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju, Kaimu Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania Bibi Lianne Houben, na Mkurugenzi wa Biashara na Kilimo wa NABC, Bw. Mackenzie Masaki.

Makampuni hayo kutoka Uholanzi ni pamoja na: Aeres University of Applied Sciences; Ebit+/I Grow Chicken; GD Animal Health; Impex; Hendrix Genetics; Koudijs de Heus; na Vencomatic Group.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Dkt. Anna Mngwira ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Kukua na Kuku akitoa neno katika sherehe za uzinduzi wa Mradi huo. Kushoto kwake ni Padri Paul Huria, Msaidizi wa Meneja Mkuu wa Kituo cha Uzalishaji na Mafunzo, Kilacha akimsikiliza kwa makini.
Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju (pichani juu) na Kaimu Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Bibi Lianne Houben (pichani chini) wakitoa hotuba fupi wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Kukua Na Kuku huko Kilacha, Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Kutoka kulia ni Padri Landelimi Makiluli, Meneja Mkuu wa Kituo cha Uzalishaji na Mafunzo, Kilacha; Padri (Monsignor) Paul Huria, Msaidizi wa Meneja Mkuu wa Kituo; Mhe. Dkt. Anna Mgwira, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro; Bibi Lianne Houben, Kaimu Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania; na mwishoni kushoto ni Mhe. Irene Kasyanju, Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi wakijiandaa na uzinduzi wa Mradi wa Kukua na Kuku
Wawakilishi wa Taasisi zenye ubia katika Mradi wa Kukua na Kuku wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiweka saini Makubaliano ya Ushirikiano tayari kuanza utekelezaji wa Mradi huo huko Kilacha, Mkoani Kilimanjaro
Picha ya pamoja baada ya kusainiwa Makubaliano ya Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania, Serikali ya Uholanzi, Makampuni tajwa 7 yakiongozwa na Mkurugenzi wa Biashara na Kilimo kutoka NABC, Bw. Mackenzie Masaki (wa pili kutoka kushoto). Wa kwanza kushoto ni Bibi Theo Mutabingwa, Afisa Kilimo katika Ubalozi wa Uholanzi nchini Tanzania.
Balozi Irene Kasyanju akibadilishana mawazo na wawakilishi wa Kampuni ya Hendrix Genetics, Bw. Peter Arts (kushoto); na Ebit+/I Grow Chicken, Bw. Eric Mooiweer (kulia) mara baada ya uzinduzi wa Mradi wa Kukua na Kuku utakaoendeshwa na Makampuni tajwa 7 kutoka Uholanzi 









Saturday, May 18, 2019

Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Jumuiya ya Mabohora.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), akiwa katika mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

Ujumbe uliombatana na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora Zainuddin Adamjee wakimuonesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki,Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), kitabu chenye picha mbalimbali zilizopiga wakati wa mkutano wa jumuiya hiyo uliofanyika Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na mabohora zaidi ya 30 elfu kutoka duniani kote ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alijumuika nao. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee na ujumbe alioambatana nae mara baada ya mazungumzo,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

Friday, May 17, 2019

Fursa za ajira

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NAFASI ZA AJIRA KATIKA SEKRETARIETI YA JUMUIYA YA MADOLA, LONDON, UINGEREZA.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inawahamasisha Watanzania wenye sifa kuomba nafasi ya ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, London, Uingereza.

Ajira hizo ni :-

Afisa Msaidizi Programu ya Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (Assistant Programmes Officer – Monitoring and Evaluation Unit) na

Meneja Utafiti wa masuala ya Uchumi, Vijana na Maendeleo Endelevu (Research Manager-Economic, Youth and Sustainable Development).

Taarifa zote muhimu kuhusu fursa hizo za ajira zinapatikana kwa kupitia  tovuti  http://thecommonwealth.org.jobs.

Mwisho wa kutuma maombi ya nafasi hizo ni tarehe 23 Mei, 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi mteule wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Sarahawi awasilisha nakala za hati za utambulisho kwa Waziri Kabudi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akipokea nakala za hati za utambulisho za Mhe. Mahayub Buyema Mahafud, Balozi mteule wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya  Sarahawi nchini Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Bwana. Mahayub Buyema Mahafud, Balozi mteule wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu Sarahawi.


Profesa Kabudi akutana na mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.)  akiwa katika mazungumzo na Mhe. Mikel Kafando ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Burkina Faso na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Mikel Kafando ambaye ni Rais Mstaafu wa Burkina Faso na Mjumbe Maalum wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (Afdb) aitembelea Tanzania




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina alipokwenda kumpokea katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.


Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serbia aitembelea Tanzania.

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Mhe.Ivica Dacic,Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serbia.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Mhe.Ivica Dacic,Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serbia na baadhi ya wajumbe aliombatana nao.


 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Mhe.Ivica Dacic, Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serbia.

 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika picha ya pamoja na Mhe.Ivica Dacic,Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serbia,wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe. 










Job Announcement at the African Union Commission

Dodoma, 17 May 2019
PRESS RELEASE

Job Announcement at the African Union Commission
The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the Commission of African Union inviting qualified Tanzanians to apply for the posts available at the Commission.

The vacant positions currently available in the commission are as follows:
Position
Department
location
Deadline
DESKTOP-PUBLISHER
DIRECTORATE OF Conference & Publication Management
Ethiopia
30/5/2019
DIRECTOR-INTER-AFRICAN BUREAU FOR ANIMAL RESOURCES ((IBAR)
Department of Rural Economy & Agriculture.
Kenya
27/5/2019
DIRECTOR-INTER-AFRICAN BUREAU FOR ANIMAL RESOURCES ((IBAR)
Department of Rural Economy & Agriculture
Kenya
30/5/2019

Details of the positions are available on the Union career website http://aucareers.org/.

Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,

Wednesday, May 15, 2019

Bid Announcement

Dodoma, 15th May 2019

PRESS RELEASE

Bid Announcement

The Republic of Mauritius invites bids from the reputable Tanzanians companies as announced by its various institutions. The interested companies can download the bidding documents from the Public Procurement Website; http://publicprocurement.govmu.org.  

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation encourages eligible companies to submit their bids on time.

Issued by:
Government Communication Unit,
 Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,

Tuesday, May 14, 2019

Nafasi za Kazi na Masomo



Dodoma, 14 Mei 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Nafasi za Kazi na Masomo

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za kazi na masomo zilizotangazwa na jumuiya za kimataifa kama ifuatavyo:

  1.     i.        Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola;

Afisa Msaidizi wa Programu katika Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (Assistant Program Officer-Monitoring and Evaluation Unit na

Meneja wa Utafiti–Uchumi, Vijana na Maendeleo Endelevu (Research Manager–Economic, Youth and Sustainable Development.
Maelezo kamili kuhusu nafasi hizi yanapatikana katika tovuti: http://thecommonwealth.org/jobs.  Mwisho wa kuwasilisha maombi ni tarehe 23 Mei 2019.

Aidha, Jumuiya ya Madola imetangaza nafasi za ufadhili wa masomo kwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo katika ngazi ya shahada ya uzamili (masters degree). Mwisho wa kuwasilisha maombi ya nafasi hizo zinazojulikana kama Queen Elizabeth Commonwealth Scholarship ni tarehe 26 Juni 2019.

Maelezo kuhusu taratibu za kuomba nafasi hizo yanapatikana kupitia tovuti: www.acu.ac.uk/scholarships/qecs.  

  1.   ii Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi (UNHCR);

Kamishina Mkuu Msaidizi wa Masuala ya Hifadhi kwa Wakimbizi (Assistant High Commissioner for Protection).

Maelezo kuhusu nafasi hii yanapatikana kupitia tovuti: https://www.unhcr.org/career-opportunities ambapo mwisho wa kuwasilisha mombi ni tarehe 20 Mei 2019 katika baruapepe recruitment.AHC-P@unhcr.org

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Monday, May 13, 2019

Prof. Kabudi ala kiapo cha utii Bunge la Afrika

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), akila kiapo cha utii mbele ya Bunge la Afrika Mashariki (EALA) ili kuwezesha kushiriki kwenye Bunge hilo  kama Waziri anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania. Tukio hilo ambalo  limefanyika kwenye Makao Makuu  ya Bunge la Afrika Mashariki jijiji Arusha leo, limeshuhudiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Spika wa Bunge hilo, Mhe. Martin Ngoga.
Sehemu ya Wabunge wa  Bunge la Afrika Mashariki wakishuhudia tukio la kuapishwa kwa Mhe. Prof. Kabudi

Mhe. Prof. Kabudi akizungumza kwenye Bunge la Afrika Mashariki mara baada ya kula kiapo cha utii cha kushiriki Bunge hilo




Sehemu nyingine ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wakifurahia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi ambaye haonekani pichani
Mhe. Prof. Kabudi akizungumza kwenye Bunge la Afrika Mashariki mara baada ya kula kiapo cha utii huku Spika wa Bunge hilo, Mhe. Martin Ngoga na wabunge wengine wakimsikiliza.