Saturday, May 18, 2019

Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Jumuiya ya Mabohora.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2019.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), akiwa katika mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

Ujumbe uliombatana na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora Zainuddin Adamjee wakimuonesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki,Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.), kitabu chenye picha mbalimbali zilizopiga wakati wa mkutano wa jumuiya hiyo uliofanyika Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na mabohora zaidi ya 30 elfu kutoka duniani kote ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alijumuika nao. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Zainuddin Adamjee na ujumbe alioambatana nae mara baada ya mazungumzo,katika ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.