Wednesday, May 1, 2019

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje washiriki maadhimisho ya Mei Mosi kwa kishindo jijini Dodoma

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (katikati) na viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (kushoto) wakiwa wamesimama kuwasalimu Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) walipopita mbele ya jukwaa kuu wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma tarehe 1 Mei 2019. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka 2019 ni  "Tanzania ya uchumi wa Kati inawezekana, wakati wa mishahara na maslahi bora ya wafanyakazi ni sasa".
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) kwa shangwe na furaha huku wakiwa wameinua juu bango lao wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi)
Sehemu ya wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho hayo
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na bango la Wizara wakati wa maadhimisho ya mei Mosi jijini Dodoma.
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho ya Mei Mosi jijini Dodoma
Ilikuwa ni shangwe na furaha kwa Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  kuadhimisha siku yao ya wafanyakazi inayoadhimishwa duniani kote tarehe 1 Mei kila mwaka
Wafanyakazi waWizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na ari katika kuadhimisha siku yao
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakijumuika na wenzao duniani kote kuadhimisha Mei Mosi

Sehemu nyingine ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Juu na chini ni umati wa Wafanyakazi kutoka Wizara, Sekta na Taasisi mbalimbali wakiadhimisha siku ya wafanyakazi duniani


Wafanyakazi wa Wizara ya Mabo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa jukwaani wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
Sehemu nyingine ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa uwanjani wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walishiriki kwa wingi kuadhimisha siku yao


Sehemu nyingine ya wafanyakazi hao wakiwa kwenye maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma
Ni nyuso za tabasamu kama zinavyoonekana kwa Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waliposhiriki kikamilifu maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
Watoto hawakuachwa nyuma na wazazi wao ambao ni Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuja kuadhimisha siku ya mfanyakazi duniani kama inavyoonekana pichani
Juu na chini ni sehemu ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiungana na wafanyakazi wengine kuimba wimbo wa mshikamano "Solidarity Forever" kama wanavyoonekana pichani


Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.