Thursday, May 9, 2019

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Mkutano wa SADC unaotarajiwa kufanyika hapa nchini mwezi August 2019,ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kupokea nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya hiyo na kutoa rai kwa Makampuni,taasisi za serikali na binafsi na wajasiriamali mbalimbali kuchangamkia fursa zitakazojitokeza wakati wa mkutano huo wa SADC.Mkutano huo wa waandishi wa habari umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakinukuu mazungumzo ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi kuhusu Mkutano wa 39 wa SADC utakaofanyika hapa Nchini mwezi August 2019 (hayupo pichani).
Sehemu ya wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na taasisi mbalimbali wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na Waandishi wa Habari Kuhusu mkutano wa SADC utakaofanyika hapa Nchini mwezi August 2019.(hawapo pichani.)
Wapiga Picha wa Vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na waandishi wa Habari kuhusu mkutano wa 39 wa SADC kufanyika hapa Nchini mwezi August 2019.






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.