Monday, May 13, 2019

Prof. Kabudi akutana na Bodii ya AICC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) kwa ajili ya kukutana na Bodi ya  Kituo hicho ikiwa ni mkutano wake wa kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo mwezi Machi 2019. Mkutano huo ulifanyika jijini Arusha tarehe 13 Mei 2019
Mhe. Prof. Kabudi akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya AICC, Balozi mstaafu,  Ladis Komba (kulia) alipokuwa akimpatia taarifa fupi kuhus bodi hiyo. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi, Balozi Brigedia Jenerali (mst.),  Francis Mndolwa  na Mkurugenzi Mwendeshaji wa AICC, Bw. Elishilia Kaaya.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.