Monday, May 13, 2019

Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na China lafanyika Arusha

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki akizungumza wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na wawekezaji kutoka Jimbo la Zhejiang la  China lililofanyika jijini Arusha tarehe 13 Mei 2019. Katika hotuba yake Mhe. Kairuki alisisitiz akuwa Tanzania ni eneo salama zaidi kuwekeza barani Afrika kutokana na sababu za msingi kama amani, mazingira na sheria rafiki za uwekezaji pamoja na maeneo lukuki ya kuwekeza kama kilimo, madini, usindikaji, viwanda na utalii. Kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Serikalini na Sekta binafsi liliwahusisha sehemu ya watalii 300 waliowasili nchini kwa ziara ya kitalii ya siku nne. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Caesar Waitara kwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jeri Muro wakifuatilia hotuba ya Mhe. Kairuki hayupo pichani


Wadau mbalimbali wakishiriki kongamano hilo


Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki naye akifuatilia matukio wakati wa kongamabo la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China lililofanyika Arusha 


Mhe. Waziri Kairuki akiendelea na hotuba yake huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Adolf Mkenda na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Gabriel Daqarro wakisikiliza


Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, Bw. GodfreySimbeye akizungumza
Mdau kutoka China naye akiwasilisha mada


Sehemu ya wawekezaji kutoka China wakifuatilia kongamano lililoandaliwa na Tanzania kwa ajili yao


Sehemu ya wadau kutoka Tanzania nao wakifuatilia kongamano


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na Mhe, Daqarro wakati wa kongamano hilo


Wadau wakifuatilia kongamano


Kongamano likiendelea




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.