Thursday, May 2, 2019

Dkt. Ndumbaro akutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na  Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), nchini leo tarehe 1 Mei, 2019, katika ofisi ndogo za wizara Kivukoni, Dar es salaam. Mazungumzo hayo, yalilenga kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na EU  kwa ajili ya mustakabali wa maendeleo ya pande hizo mbili. Baadhi ya masuala yaliyojadiliwa ni pamoja na Mkataba wa Ubia wa Kiuchumi katika ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ushirikiano katika nyanja za elimu na udhibiti wa biashara haramu ya dawa za kulevya. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.), akifafanua jambo wakati wa mazungumzo hayo.
Kaimu Balozi Stuart akielezea jambo wakati wa mazungumzo hayo.
Afisa Mambo ya Nje  wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Albert Philipo akifuatilia mazungumzo hayo.
Juu na chini mazungumzo yakiendelea.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.) akiagana na Kaimu Balozi Charles Stuart mara baada ya mazungumzo.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.