Friday, July 26, 2024

BALOZI KOMBO NA MANAIBU WAKE WAPOKELEWA KATIKA OFİSİ NDOGO ZA WIZARA DSM

 


 

 





















 

 

 

 

 

 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amewasili na kupokelewa katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam akitokea Ikulu ya Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa Waziri na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Katika mpokezi hayo, Mhe. Balozi Kombo aliiambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Lazaro Londo na kulakiwa kwa bashasha na viongozi na Watumishi wa Wizara waliokusanyika katika Ofisi ndogo, Dar Es Salaam.


Mhe. Balozi Kombo pamoja na Naibu Mawaziri, Mhe. Londo na Mhe. Chumi waliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kushika nyadhifa hizo katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Julai 21, 2024

 

RAIS SAMIA AWAAPISHA MHE. BALOZI KOMBO NA MANAIBU WAZIRI IKULU DAR ES SALAAM

Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo akiapa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu Dar es Salaam, Julai 26, 2024

Mhe. Dennis Lazaro Londo akiapa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Masharika, Ikulu Dar es Salaam, Julai 26, 2024


Mhe. Cosato Chumi akiapa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu Dar es Salaam, Julai 26, 2024



Mawaziri na Manaibu Waziri Wakiapa kiapo cha Uadilifu baada ya kuapishwa na Mhe. Rais  kushika nyadhifa hizo Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2024.


Mawaziri na Manaibu Waziri wakisaini Hati ya kiapo cha Uadilifu baada ya kula kiapo hicho na kuapishwa na Mhe. Rais  kushika nyadhifa hizo Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2024.

 

Thursday, July 25, 2024

DKT. TULIA AMUAPISHA BALOZI MAHMOUD THABIT KOMBO KUWA MBUNGE

 




 







 

 

 

 




Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Akson amemuapisha Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla ndogo iliyofanyika Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam tarehe 25 Julai,2024.

Hafla hiyo ya uapisho imehudhuriwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Naibu Waziri Mteule wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Lazaro Londo, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Naibu Katibu Mkuu Balozi Said Shaib Mussa na watendaji wengine wa Ofisi ya Bunge.

Tarehe 21 Julai, 2024 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alimteua Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Mhe. Rais pia aliwateua Mhe. Dennis Lazaro Londo (Mb) kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mhe. Cosato David Chumi (Mb) kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje. Waziri.

 Mhe. Balozi Kombo na Manaibu Waziri wateule wataapishwa tarehe 26 Julai, 2024 Ikulu jijini Dar es salaam.

Wednesday, July 24, 2024

TANZANIA-COMORO ZASAINI HATI NNE ZA MAKUBALIANO


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro anayeshughulikia Nchi za Kiarabu, Nchi zinazozungumza Kifaransa, Diaspora na Mtangamano wa Afrika Mhe. Mohamed Mbae wakionesha moja ya Hati za Makubaliano.

Tanzania na Visiwa vya Comoro zimesaini Hati nne za Makubaliano kwenye kilele cha Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro uliofanyika tarehe 24 Julai,2024 jijini Dar es Salaam. 

Hati zilizosainiwa katika kikao hicho zinazojumuisha nyanja za; Ushirikiano wa Kidiplomasia, Afya, Biashara na Viwanda na Teknolojia ya Habari. Utiaji saini hati hizo umeshuhudiwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro anayeshughulikia Nchi za Kiarabu, Nchi zinazozungumza Kifaransa, Diaspora na Mtangamano wa Afrika Mhe. Mohamed Mbae.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo wa kihistoria, Waziri Tax ameelezea umuhimu wa kusainiwa kwa hati hizo kuwa itawezesha pande hizo mbili kuwa na ushirikiano ulio katika mpangilio mzuri katika nyanja husika na hivyo kuleta tija zaidi.

"Pamoja na kutia saini Hati za Makubaliano pia tumekubaliana kuendelea kushirikiana katika maeneo mengine mengi ikiwemo miondombinu, nishati, ulinzi na usalama, uchumi wa buluu, utalii, utamaduni, sanaa na michezo na Maendeleo ya vijana". Ameeleza Dkt. Tax


Naye Mhe. Mbae ameeleza kufurahishwa kwake na kufanyika kwa mkutano huo wa JPC na kuongeza kuwa mkutano huo ni kiungo muhimu katika kuendelea kukuza na kuimarisha uhusiano na kati ya Tanzania na Comoro.

Ameipongeza Tanzania kwa kuandaa mkutano huo na hivyo kuonesha dhamira ya dhati ya Tanzania katika kuendelea kushirikiana na Comoro.

Mbali na kusainiwa kwa Hati hizo Mawaziri hao wameridhishwa na kupongeza hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa makubaliano na maamuzi mbalimbali yaliyofikiwa kwa pamoja kati ya pande hizo mbili tangu kusainiwa kwa Mkataba wa Jumla wa Ushirikinao mwaka 2009. 

Vilevile mkutano huo umejadili na kuweka mikakati ya namna ya kuendelea kukuza biashara baina ya pande hizo mbili. Mikakati hiyo pamoja na mambo mengine italenga kuwahimiza sekta binafsi kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili na kuchangamkia fursa za kibiashara zilizopo na zile zinazotokana na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) na Eneo Huria la Biashara la SADC.

Akizungumzi kuhusu mkutano huo Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu ameeleza kuwa, Comoro ni mshirika muhimu wa Tanzania katika biashara, ambapo kwa mwaka 2023 Tanzania iliuza nchini humo bidhaa zenye thamani ya shilingi bilioni 148. 

Ameongeza kusema kuwa makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano huo sio tu yataongeza ushirikiano wa kidiplomasia bali yanatarajiwa kuongeza kiasi cha bidhaa ambazo Tanzania inaingiza nchini humo. 

Katika mkutano huo ujumbe wa Tanzania umejumuisha wataalamu na watendaji kutoka sekta mbalimbali na umeongozwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax, ambaye pia aliongoza mkutano huo kwa kushirikiana na mwenyekiti mwenza Waziri Mbae wa Comoro. 
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitoa hutoba ya ufunguzi kwenye Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro uliofanyika tarehe 24 Julai,2024 jijini Dar es Salaam
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitoa hutoba ya ufunguzi kwenye Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro uliofanyika tarehe 24 Julai,2024 jijini Dar es Salaam
Washiriki wa Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro wakifurahia jambo

Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro uliofanyika tarehe 24 Julai,2024 ukiendelea jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro anayeshughulikia Nchi za Kiarabu, Nchi zinazozungumza Kifaransa, Diaspora na Mtangamano wa Afrika Mhe. Mohamed Mbae wakitia saini Hati za Makubaliano
Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro anayeshughulikia Nchi za Kiarabu, Nchi zinazozungumza Kifaransa, Diaspora na Mtangamano wa Afrika Mhe. Mohamed Mbae akizungumza kwenye Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Comoro uliofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaibu Mussa akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro uliofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaibu na Mhe. Balozi Fatima Alfeine wa Comoro wakifuatilia zoezi la utiaji saini wa Hati za Makubaliano kwenye mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro unaofanyika jijini Dar es Salaam

DKT. TAX AKUTANA NA KAIMU NAIBU WAZIRI WA MAREKANI

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akisalimiana na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass alipokutana naye kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Batle  alipomsindikiza Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaamm, kulia ni Katibu Mkuu Balozi Shelukindo akisalimiana na Balozi wa Marekani Mhe. Michael Batle 
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akizungumza na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


 Katibu Mkuu Balozi Samwel Shelukindo (kushoto) akiwa na watumishi wa wizara katika kikao kati ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb)  Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass alipofika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Batle (kulia) akiwa na ujumbe wake  katika kikao kati ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb)  Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass alipofika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb)  akiwa na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass alipofika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb)  akiwa na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass  pamoja na Katibu Mkuu Balozi Samwel Shelukindo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Batle (kulia) alipofika  katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass katika picha ya pmoja baada ya kumaliza mazungumzo yao  katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam







Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena L. Tax (Mb), amekutana kwa mazungumzo na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho Dkt. Tax amemuhakikishia Mhe. Bass kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Marekani katika masuala yenye manufaa kwa nchi hizi mbili na wananchi wake.

Amesema ziara ya Mhe. Bass nchini ni ushahidi wa  uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizo mbili huku ikonesha umuhimu mkubwa katika kuendelea kudumisha na kuimarisha maelewano, ushirikiano na urafiki kati ya Tanzania na Marekani na kuongeza kuwa kwa miaka mingi kumekuwa na majadiliano ya wazi kwa ajili ya kujenga na kuweka misingi ya ushirikiano madhubuti kati ya Tanzania na Marekani.

“Nina Imani kuwa kupitia ushirikiano na uhusiano wetu sio kwamba tutakabiliana na changamoto zinazotukabili kwa pamoja bali pia tutanufaika na fursa zilizopo mbele yetu ili kuchochea ukuaji na ustawi wa pamoja, alisema Dkt. Tax.

Naye Mhe. Bass akizungumza katika kikao hicho amesema ziara yake nchini ina lengo la kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano na Tanzania na kuahidi kuwa Marekani inaiona Tanzania kama mdau wa kimkakati katika ushirikiano wa maendeleo.

Ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kufanya kazi kwa pamoja na Serikali ya Marekani na kuongeza kuwa ni matarajio yake kuwa kupitia majadiliano mbalimbali ambayo yemekuwa yakifanyika yatasaidia nchi yake kuibua kwa undani maeneo muhimu ambayo Serikali ya Tanzania inahitaji kuendelea ushirikiana na Marekani. 

Tanzania na Marekani zimekuwa zikishirikina katika nyanja za afya kupitia miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Shirika la Misaada la USAID, elimu, kilimo, biashara na uwekezaji, ulinzi na usalama.

Tuesday, July 23, 2024

MKUTANO WA 117 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA JUMUIYA YA NCHI ZA AFRIKA, CARIBBEAN NA PASIFIKI (OACPS) WAANZA JIJINI BRUSSELS

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo wa 117 ulioanza tarehe 23 Julai 2024, kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Bw. Msafiri Mbibo akifuatilia mkutano huo. 


Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 

Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 

Maafisa waandamizi wa Serikali wakifuatilia Mkutano huo 


Mkutano ukiendelea 

Mkutano ukiendelea  kutokea jijini Brussels


Mkutano ukiendelea  kutokea jijini Brussels



Mkutano wa 117 wa Baraza la Mawaziri la nchi za nchi za Jumuiya ya nchi za Afrika, Caribbean na Pasifiki (OACPS) Unachofanyika kwa mfumo wa mseto kuanzia tarehe 23 hadi 26 Julai 2024 umeanza jijini Brussels, Ubelgiji. 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede , anaongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo wa 117 ulioanza tarehe 23 Julai 2024. 

Mkutano huo pia unafuatiliwa kwa njia ya mtandao na Balozi wa Tanzania Brussels Mhe. Jestas Nyamanga na Maafisa waandamizi kutoka Wizara za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha, Viwanda na Biashara, Uvuvi, Mifugo, Madini, na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mkutano huo wa kwanza kwa mwaka huu unajadili maendeleo muhimu ya ushirikiano kati ya wanachama katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa pamoja na kuwa jukwaa la kuboresha mikakati ya kikanda na kimataifa ili kuimarisha maendeleo endelevu na ushirikiano wa kimaendeleo kati ya nchi za OACPS. 

Mkutano huo pia utatoa fursa ya kuimarisha uhusiano na Umoja wa Ulaya kupitia majadiliano ya Mkataba wa Ushirikiano wa Samoa ambao unalenga kuboresha biashara uwekezaji na ushirikiano wa kisiasa kati ya nchi za OACPS na Umoja wa Ulaya.

Mkutano huo unatarajiwa kujadili na kupitisha bajeti ya OACPS kwa mwaka 2024, kupitia na kujadili taarifa za fedha za OACPS ikiwemo taarifa ya uchaguzi wa hesabu za Jumuiya, kujadili utekelezaji wa Mkataba wa Ubia  kati ya OACPS na Umoja wa Ulaya kuhusu mkataba wa Samoa, kujadili taarifa ya ununuzi wa jengo jipya la Ofisi za OACPS na kujadili taarifa ya mkutano wa Mawaziri wa Madini na Nchi za OACPS uliofanyika Cameroun kuhusu uendelezaji wa madini ya kimkakati kwenye nchi wanachama.

Mkutano huo wa Baraza la Mawaziri hukutana mara mbili kwa mwaka kujadili na kuamua kuhusu masuala mbalimbali ya jumuiya ni jukwaa muhimu kwa Mawaziri wa nchi hizo kubadilishana mawazo na kufanya maamuzi kuhusu matukio na maendeleo muhimu yaliyotokea katika kipindi cha kuanzia Juni 2023 hadi Juni 2024 ambako masuala na fursa muhimu zinazohitaji uelewa wa pamoja na mwelekeo wa kimkakati wa Mawaziri wa OACPS yalitokea.

Wajumbe wa sasa wa Baraza hilo la Mawaziri linaundwa na nchi za Jamaica- Rais, Liberia- Rais anayeondoka, Jamhuri ya Kongo, Rais ajaye, Sudan- Inawakilisha Afrika Mashariki, Angola Inawakilisha Kusini mwa Afrika, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-Inawakilisha Afrika ya Kati, Burkina Faso, Inawakilisha Afrika Magharibi,Haiti Inawakilisha nchi za Karibiani na Vanuatu Inawakilisha nchi za Pasifiki.