Wednesday, September 4, 2024

HATI YA MAKUBALIANO YA KUBORESHA RELI YA TAZARA YASAINIWA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping na Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema kwa pamoja wameshuhudia uwekaji saini wa hati ya makubaliano (MoU) ya kuboresha reli ya TAZARA uliofanyika katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.

Kwa upande wa Tanzania zoezi la uwekaje saini limefanywa na Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping pamoja na Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakishuhudia uwekaji saini wa hati ya makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.