Wednesday, September 25, 2024

NAIBU WAZIRI CHUMI NA BALOZI WA JAPAN WAKUTANA JIJINI DODOMA


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akisalimiana na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi Misawa walipo akutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi amekutana na Balozi wa Japan nchini Mhe. Yasushi Misawa aliyemtembelea ofisini kwake Jijini Dodoma. 

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Japan kwa manufaa ya pande zote.

Mhe. Chumi aliishukuru Serikali ya Japan kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kupitia sekta mbalimbali na hivyo kuunga mkono jitihada za Serikali katika kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Mhe. Chumi pia amemhakikishia Mhe. Balozi Misawa kuwa Tanzania inajali na kuthamini uhusiano wake na Japan na kumuahidi kuwa Mamlaka ya Biashara Nje (Tantrade) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Japan wanaendelea na maandalizi ya kushiriki katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara yatakayofanyika Osaka nchini Japan mwaka 2025.

Naye Balozi wa Japan Mhe. Misawa ameelezea utayari wa nchi yake kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa manufaa ya pande zote mbili.

Pia ameshukuru Ushirikiano anaoupata kutoka Serikali ya Tanzania na hivyo kumuwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Tanzania na Japan zinashirikiana kupitia sekta za biashara na uwekezaji, miundombinu, afya na masuala ya kodi.
Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi Misawa akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi yaliyofanyika jijini Dodoma. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi Misawa yaliyofanyika jijini Dodoma.
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.