Tuesday, September 24, 2024

Waziri Kombo ashiriki kwenye Mkutano wa Nchi za Jumuiya ya Madola (Commonwealth Foreign Affairs Ministers Meeting - CFAMM)



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Thabit Kombo (Mb.) ameshiriki kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Jumuiya ya Madola (Commonwealth Foreign Affairs Ministers Meeting - CFAMM) uliofanyika pembezoni mwa Kikao cha 79 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79) tarehe 23 Septemba, katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York. 

 

Kikao hicho kilicho hudhuriwa na Mawaziri kutoka nchi 56 za Jumuiya ya Madola kilijadili ajenda mbalimbali, zikiwemo taarifa ya utekelezaji wa maelekezo ya Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Nchi za Jumuiya ya Madola (CHOGM) uliofanyika mwaka 2022, Kigali, Rwanda na taarifa ya maandalizi ya Mkutano ujao wa CHOGM, utakaofanyika mwezi Oktoba 2024, Apia, Samoa.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.