Monday, September 30, 2024

NJE - SPORTS YAICHAPA MIFUGO KWA PENATI 6-5


.Yaifundisha mifugo diplomasia ya michezo 

. Yatinga nusu fainali 

Timu ya Soka ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje - Sports), yaichapa Timu ya Mifugo kwa penati 6-5 katika mchezo wa nusu fainali ya michezo ya Shimiwi inayofanyika mjini Morogoro.

Hadi dakika 90 zinakamilika timu hizo zilikuwa zimefungana goli    1 – 1 na kulazimika kupigiana mikwaju ya penati.

Katika kupigiana mikwaju ya penati, Nje Sports ilitumia umahiri wake wa Diplomasia ya Michezo kupachika kimiani mikwaju Sita bila kumjeruhi Mlinda Mlango wa timu ya Mifugo Bwana NKANA ambapo Mlinda Mlango wa Nje – Sports Bw. Deusi Benedictor alipangua mikwaju miwili ya penati kwa Ustadi wa hali ya juu na kuisukuma nje ya mashindano kwa kishindo Timu ya Mifugo.

 Mwenyeki wa Michezo wa Wizara na team ya Nje – Sports Bwa. Ismail  H.Abdallah alionekana kuwa na furaha  baada ya Timu ya Wizara ya Mambo ya Nje kuibuka na Ushindi huo.

 “Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata Ushindi ambao tulikuwa tunatamani,  nashukuru timu imepambana, ahadi tuliyo muahidi Katibu Mkuu tumeitimiza kwa kuingia Nusu fainali”, alisema Bw. Ismail.

Bw. Ismail ametoa rai kwa wanamichezo wa Nje Sports  kujituma na kujitoa kwani kupitia michezo hiyo wanaonesha Diplomasia ya Michezo pia kuionesha jamii kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Afrika Mashariki inafanya vizuri pia kwenye anga za michezo.

Aidha, Kocha  Maganga na wachezaji wake wametoa pongezi kwa Katibu Mkuu kwa namna alivyowapa hamasa iliyopelekea kufanya vizuri kwenye michezo hiyo ya Shimiwi.

Kocha huyo wa Nje sports amewaalika viongozi wa Wizara kwenda kuiona Timu yao itakaposhuka kwenye mchezo wa Nusu Fainali utakaofanyi baada ya ratiba kutolewa.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.