Tuesday, October 1, 2024

NAIBU WAZIRI LONDO AWAPONGEZA NJE – SPORTS KWA KUFANYA VIZURI SHIMIWI


 NAIBU WAZIRI LONDO AWAPONGEZA NJE – SPORTS KWA KUFANYA VIZURI SHIMIWI

 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Denis Londo amewapongeza wanamichezo wa timu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje - Sports), kwa kufanya vizuri katika michezo ya SHIMIWI inayoendelea mjini Morogoro.

Mhe. Londo amezipongeza Timu ya Mpira wa miguu wanaume kwa kuingia Nusu fainali , Timu ya Kamba wanawake na Timu ya Mpira wa pete kwa kuingia 16 Bora ya michuano ya SHIMIWI yanayoendelea Mkoani Morogoro

 Mhe. Londo ametoa pongezi hizo tarehe 30 Septemba, 2024 alipokutana na wachezaji wa Nje – Sports katika hafla ya Chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa ajili yao mjini Morogoro. 

Hafla hiyo imefanyika maalum kuwapa hamasa wachezaji ili waendelee kufanya vizuri kwenye michuano hiyo. 

Katika hafla hiyo Mhe. Londo alifikisha salam za Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Thabit Kombo ambaye aliwataka wachezaji hao waendelee kupambana hadi mwisho.

 “Nilimweleza Mhe. Waziri kuwa naenda Mikumi lakini nitarudi jioni kwa ajili ya chakula cha jioni na Ninyi. amefurahia na ameniambia niwaletee salamu za upendo na kusema kwamba yupo pamoja na ninyi na muendelee kupambana hadi mwisho na anawatakia kila la kheri” Amesema Mhe. Londo

 Naye Mwenyekiti wa Michezo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Ismail Abdallah, ameupongeza na kuushukuru uongozi wa Wizara kwa namna wanavyo wapa miongozo na namna wanavyo wapa hamasa ambayo imekuwa chachu ya wao kufanya vizuri kwenye michezo hiyo.  

Pia amempongeza Naibu Waziri Mhe. Londo kwa kufika uwanjani kujionea pamoja na kuzungumza na wachezaji kitu kilichowapa hamasa kubwa wachezaji na kupelekea kufanya vizuri kwenye mchezo wao.

 “Mafanikio haya Mheshimiwa yamechagizwa sana na kitendo ulichokifanya juzi, kitendo cha kutenga muda wako na kuja kututembelea na hukuja kambini bali umekuja Uwanjani, kwakweli toka tumefika hapa sidhani kama kuna Timu Waziri wao amekuja kuwatembelea kama ulivyo fanya, kwakweli umetujengea hamasa kubwa, heshima kubwa mpaka tumeonekana Watoto pendwa sijui nitumie neno gani lakini tumeonekana wakipekee. Tunashukuru sana” Amesema Bwa. Ismail

 Nje – Sports inatarajia kuingia dimbani hapo kesho kwa Mchezo wa Nusu Fainal dhidi ya mpinzani Wake Wizard ya Maji.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.