Sunday, October 20, 2024

MHESHIMIWA PINDA AWASILI GABORONE KUONGOZA MISHENI YA SADC YA UANGALIZI UCHAGUZI NCHINI BOTSWANA

 

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Botswana mwenye makazi yake Afrika Kusini Mhe. James Bwana alipompokea katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama wa Gaborone, alipowasili kuongoza Misheni ya SADC ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Botswana uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Botswana mwenye makazi yake Afrika Kusini Mhe. James Bwana alipompokea katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama wa Gaborone, alipowasili kuongoza Misheni ya SADC ya Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Botswana uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024
 
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda akiwa katika chumba cha mapumziko alipowasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama wa Gaborone,  kuongoza Misheni ya SADC ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Botswana uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama wa Gaborone kuongoza Misheni ya Uangalizi Uchaguzi ya SADC nchini Botswana

Mwakilishi wa Mratbu wa Masuala ya SADC Tanzania bi. Lilian Mukasa (aliyesimama) akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mkuu wa Misheni ya SADC Uangalizi Uchaguzi Mkuu wa Botswana Mhe. Mizengo Pinda alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama, Gaborone kuongoza Misheni ya Uangalizi Uchaguzi ya SADC nchini Botswana

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa akimkabidhi  nyaraka mbalimbali Waziri Mkuu Mstaafu na Mkuu wa Misheni ya SADC Uangalizi Uchaguzi Mkuu wa Botswana Mhe. Mizengo Pinda  alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama wa Gaborone kuongoza Misheni ya Uangalizi Uchaguzi ya SADC nchini Botswana

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda  katika picha ya pamoja na viongozi waliofika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama jijini Gaborone , Botswana kwa ajili ya kuongoza Misheni ya SADC ya Uangalizi Uchaguzi Mkuu wa Botswana utakaofanyika tarehe 30 Oktoba, 2024





Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda amewasili jijini Gaborone, Botswana tarehe 19 Oktoba, 2024.
 

Mhe. Mizengo Pinda ataongoza Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC- SEOM) katika Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Botswana uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba, 2024.

Katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Sir Seretse Khama jijini Gaborone Mhe. Pinda amelakiwa na Balozi wa Tanzania nchini Botswana mwenye makazi yake Afrika Kusini Mhe. James Bwana.

Mhe. Pinda ataongoza SEOM kufuatia kuteuliwa kuongoza Misheni hiyo na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC (Troika) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Pinda atazindua rasmi Misheni ya SEOM inayoundwa na wajumbe kutoka Nchi Wanachama wa SADC tarehe 22 Oktoba, 2024.

Mhe. Pinda kwa kushirikiana na Wajumbe wengine wa Troika (Zambia na Malawi) atakutana na wadau mbalimbali wa uchaguzi ikiwemo Tume ya Uchaguzi ya Botswana (IEC), Mabalozi wa Nchi za SADC waliopo Botswana, Vyama vya siasa, Asasi za Kiraia, Taasisi za dini na Vyombo vya Habari kwa ajili ya kuelezea kazi ambayo SEOM itafanya katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu  hadi kukamilika kwake.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.