Thursday, September 19, 2024

NJE - SPORTS YAJIGAMBA KUFANYA VYEMA KWENYE MASHINDANO YA SHIMIWI - MOROGORO


Ratiba ya makundi katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayoanza kufanyika mkoani Morogoro imetolewa hadharani, huku Timu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Wanaume (Nje-Sports) inatarajia kurusha karata yake ya kwanza tarehe 21 Septemba, 2024 kwa Kuvaana na Timu ya Ras Mara.

Mwenyekiti wa Nje - Sports Bw. Ismail Abdallah amesema kuwa katika mpira wa miguu, timu ya Nje Sports imepangwa kundi G pamoja na timu za Utumishi, Wizara ya Ujenzi, Ras Mara na Ras Lindi.

Ameeleza pia kuwa timu ya Nje – Sports Kamba (Ke) imepangwa katika kundi B na itapepetana na timu za Hazina, Kilimo na Ras Shinyanga, huku mpira wa Pete ikipangwa kundi H na itaumana na Mahakama, Maadili, na Ras Lindi.

Kwa upande wa Kocha wa Nje – Sports, Bw. Shabani Maganga amesema vijana wote wapo salama na wapo tayari kupambana katika mashindano hayo ili kuibuka na ushindi kwenye kila mchezo kutokana na ubora wa timu waliyonayo.

Leo jioni tarehe 19 Septemba, 2024, Nje Sports imeendelea kufanya mazoezi mepesi ya kujiandaa na mashindano hayo ambayo yanatarajiwa kuanza kesho tarehe 19 Septemba, 2024.

Nje - Sports inayoshiriki katika michezo mbalimbali mwaka huu, ikiwemo Mpira wa Miguu Wanaume, Kamba wanawake, Mpira wa Pete, Bao, Karata, iliwasili mkoani Morogoro jumatatu tarehe 16 Septemba, 2024 na kuzua gumzo kwenye viunga na mitaa mbalimbali ya mjini Morogoro (Mji kasoro Bahari).



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.