Thursday, September 26, 2024

NJE – SPORTS YAPONGEZWA NA UONGOZI NA MENEJIMENTI YA WIZARA


Timu ya michezo ya Wizara ya Mambo ya. Je na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports Club) imepongezwa kwa kuendelea kufanya vizuri katika michuano ya 38 Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) inayoendelea Mkoani Morogoro.

Pongezi hizo zimewasilishwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (ADA) Bw. Kawina Kawina alipotembelea na kuzungumza na wachezaji wa timu hiyo walioweka kambi kwenye milima ya Uluguru.

 Katika mazungumzo na wachezaji hao Bw. Kawina kwa niaba ya Uongozi na Menejimenti ya Wizara amewapongeza wachezaji kwa kuendelea kufanya vizuri katika michezo ya SHIMIWI na kuwahakikishia kuwa wizara ipo pamoja nao kwenye kila hatua wanayopiga katika michezo hiyo.

 “Uongozi na Menejimenti ya Wizara umekuwa ukipata taarifa kupitia Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali (GCU), kuwa Nje – Sports inafanya vizuri kwenye michezo ya SHIMIWI inayoendelea hapa Mkoani Morogoro,” alisema Bw. Kawina.

 Aliongeza kuwa, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo anamatumaini makubwa na na timu hiyo na matarajio ya Wizara ni kuwa wataibuka na ushindi na kurejea na Vikombe.

 Bw. Kawina pia amewapongeza wanamichezo wote kwa kuendelea kuwa waadilifu na kuonyesha nidhamu huku wakizingatia Kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma wakati huu wa Michezo ya SHIMIWI na kuwa chachu ya kuzifikisha Timu zote tatu za Nje Sports katika hatua ya 16 Bora.

Akizungumza katika kikao hicho na Mkurugenzi Kawina  Kapteni wa Mpira wa Miguu Bw. Mikidadi Magola ameishukuru Wizara kwa namna inavyokabiliana na changamoto zinazoikabili  timu ya Nje  na kuiwezesha Timu kupata vifaa vyote vya mühimu kwa timu hiyo  ambavyo vimekuwa chachu ya kufanya vizuri kwenye michezo ya SHIMIWI mwaka huu.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.