Friday, September 20, 2024

NJE - SPORTS Netiboli YAANZA VIZURI SHIMIWI, YAIBAMIZA RAS LINDI

 


Timu ya netiboli ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje - Sports) imeanza kwa kishindo Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) baada ya kuitandika bila huruma Timu ya Ras Lindi kwa magoli 39 -16.

 

Kama wahenga wasemavyo Nyota njema huonekana asubui, katika mchezo huo nyota ya Nje - Sports Netiboli ilianza kuangaza tangu kipenga cha mwamuzi wa mchezo kilivyopulizwa, ikionyesha ustadi wao wa hali ya juu.

 

Akizungumza mara baada ya ushindi huo, Kapteni wa Netiboli Nje – Sport Bi. Faraja Kessy, amesema ushindi huo umetokana na maandalizi mazuri ya muda mrefu, hata hivyo mchezo ulikuwa na ushindani Mkubwa sana lakini tumeibuka na Ushindi Mnono. 

 

"Hakika tunafuraha sana kwa kuanza vizuri katika mchezo wetu wa kwanza wa netiboli. Na matarajio yetu ni kuendelea kufanya vyemza zaidi na kuweza kuibuka washindi katika Michezo hii ya SHIMIWI”. 

 

Vilevile, Bi. Faraja Kessy ameushukuru Uongozi na menejimenti ya Wizara kwa ujumla kwa namna ambavyo wamekuwa mstari wa mbele kutoa hamasa kwa wanamichezo na kuahidi kuendelea kufanya vyema katika michezo iliyobakia katika kundi letu.

 

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Michezo Nje – Sports, Bw. Ismail Abdallah ameendelea kuwapongeza na kuwapa hamasa zaidi wana michezo woote. “Kwakweli leo Mambo yako mazuri nifuraha sana kuona tokea asubui tunapata ushindi tuu”.

 

Kesho Tarehe 21 Septemba, 2024 Nje – Sports wanawake wanatarajia kurusha karata yao ya pili ambapo watamenyana na Mahakama, kwa upande wa Mpira wa Miguu Nje – Sports wanashuka dimbani kucheza mchezo wao wa kwanza ambao watachuana na Utumishi.









Nifuraha kweli kweli.







No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.