Wednesday, February 18, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi kutoka Malawi, Kuwait, Afrika Kusini na Kenya


...Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Malawi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambuliosho kutoka kwa Balozi mpya wa Malawi hapa nchini, Mhe. Hawa Olga Ndilowe. Balozi Ndilowe amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Marehemu Balozi Flossie Gomile-Chidyaonga aliyefariki ghafla mwezi Mei 2014. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 18 Februari, 2015
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Ndilowe mara baada ya kupokea Hati zake za Utambulisho
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha  na Balozi Ndilowe pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)  (mwenya tai ya bluu) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum, Mhe. Prof. Mark Mwandosya (wa kwanza kulia) pamoja na baadhi ya Maafisa kutoka Ubalozi wa Malawi hapa nchini.
Balozi Ndilowe akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kabla ya kukabidhi Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Kikwete
Balozi Ndilowe akisikiliza wimbo wa taifa lake uliopigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kukabidhi Hati za Utambulisho. Kulia ni Balozi Mohamed Maharage Juma , Mkuu wa Itifaki na Kaimu Mnikulu, Bw. Fyataga
Brass Band ya Polisi wakipiga wimbo wa taifa wa Malawi kwa heshima ya Balozi Ndilowe.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Itifaki, Bw. James Bwana wakati wa mapokezi ya Balozi mpya wa Malawi hapa nchini Mhe. Ndilowe.
Maafisa kutoka Ubalozi wa Malawi hapa nchini wakiwa na Bi. Mercy Kitonga, Afisa Mambo ya Nje wakifutilia taratibu za mapokezi ya Balozi Ndilowe (hayupo pichani)
Balozi Ndilowe akiagana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho kwa Balozi.

...Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Kuwait

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambuliosho kutoka kwa Balozi mpya wa Kuwait  hapa nchini, Mhe. Jasem Ibrahim Al-Najem. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 18 Februari, 2015.
Balozi Al-Najem akisalimiana na Waziri Membe mara baada ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Kikwete
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Balozi Al-Najem
Mhe. Rais Kikwete na Balozi Al-Najem katika picha ya pamoja na Waziri Membe, Prof. Mwandosya na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya (kulia)
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika mazungumzo na Balozi Al-Najem
Balozi Al-Najem akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu
Balozi Al-Najem akisikiliza wimbo wa taifa lake wakati wa mapokezi yake Ikulu.
Bendi ya Polisi ikipiga wimbo wa Taifa wa Kuwait na Tanzania


...Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Afrika Kusini



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambuliosho kutoka kwa Balozi mpya wa Afrika Kusini hapa nchini, Mhe. Thamsanqa Dennis Mseleku. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 18 Februari, 2015.
Balozi Mseleku akisalimiana na Waziri Membe
Balozi Mseleku akisalimiana na Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Balozi Yahya huku Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akishuhudia


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (kulia) pamoja na Bi. Talha Mohamed na Bw. Mudrick Soragha wakifuatilia kwa makini tukio la uwasilishaji Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Afrika Kusini hapa nchini (hayupo pichani)


Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Mseleku mara baada ya kupokea hati zake za utambulisho.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salva Rweyemamu (kulia) akiwa na Mshauri wa Rais masuala ya Diplomasia, Balozi Samwel Shelukindo (kushoto) na Bi. Bundala wakinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Balozi Mseleku (hawapo pichani)

...Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Kenya


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambuliosho kutoka kwa Balozi mpya wa Kenya hapa nchini, Mhe. Chirau Ali Mwakwere. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 18 Februari, 2015.
Mhe. Rais Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na Balozi Mwakwere
Picha ya pamoja






Tuesday, February 17, 2015

Naibu Waziri mgeni rasmi ufunguzi wa Taasisi ya Sheria za Kimataifa

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akitoa hotuba ya ufunguzi rasmi wa Taasisi ya Sheria za Kimataifa ya Afrika-AIIL yenye Makao Makuu yake Jijini Arusha hivi karibuni.
Sehemu ya Wajumbe akiwemo Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju (wa pili kulia) wakimsikiliza Mhe. Maalim (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Taasisi hiyo.
Mhe. Maalim (wa tano kushoto walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe waliohudhuria ufunguzi rasmi wa Taasisi ya Sheria za Kimataifa ya Afrika iliyopo Arusha.
Mhe. Maalim akifafanua masuala mbalimbali kuhusu Taasisi hiyo kwa Waandishi wa Habari

Monday, February 16, 2015

Balozi Dkt. Aziz Ponary Mlima awasilisha Hati za Utambulisho nchini Laos

Dkt. Aziz Ponary Mlima Balozi wa Tanzania nchini Malaysia akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Laos Mheshimiwa Choummaly Sayasone. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni mjini Vientiane nchini Laos.
Dkt Aziz Mlima akifanya mazungumzo na Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Laos ambaye aliwahi kuwa Balozi wa Laos kwenye Umoja wa Mataifa kwa muda mrefu Mheshimiwa Alounkeo Kittikhoun.Ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia unawakilisha nchi nyingine 6 katika ukanda wa Kusini Mashariki mwa Asia.

Sunday, February 15, 2015

Waziri Membe mgeni rasmi kwenye sherehe za kuukaribisha mwaka Mpya waKichina

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akipokelewa kwa furaha na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing alipowasili katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya wa Kichina. Waziri Membe amemwakilisha Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwenye hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam







Waziri Membe akisalimiana na Brigedia Genral. Rogastian Laswai, Mkuu wa Kikosi cha wanamaji nchini
Waziri Membe akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Said Meck Sadiq mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mmnazi mmoja.

Waziri Membe akisalimiana na Mkurugenzi wa Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) Bibi. Julieth Kairuki
Mhe. Membe pamoja na Balozi Lu Youqing wakiimba wimbo wa Taifa katika Hafla ya kuukaribisha mwaka mpya wa Kichina
Waziri Membe akitoa Salaam za pongezi za kuadhimisha mwaka mpya wa Kichina kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Pia Mhe. Membe alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya china katika kudumisha uhusiano mzuri baina ya Tanzania na China katika nyanja ya Uchumi, Siasa na kijamii.


Balozi Youqimg(Wakwanza kushoto), Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq (Wapili kutoka kushoto), Naibu Balozi wa China nchini, na wanne kutoka kushoto ni Mkurugenzi Idaya ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe akihutubia katika Hafla hiyo iliyoandaliwa na Ubalozi wa China nchini.
Waziri Membe akiendelea kuhutubia
Wachina waishio nchini Tanzania wakifuatilia kwa makini Hotuba kutoka kwa Mhe. Waziri
Sehemu ya Viongozi mbalimbali kutoka Jeshi la Wananchi la Tanzania walioudhuria katika Hafla hiyo 
Kikundi cha maonyesho ya Utamaduni wa Jamhuri ya watu wa China kikisherehesha
Waziri Membe akifurahia onyesho  lililokuwa likiendelea kuonyesha na kikundi cha nyimbo za tamaduni za Kichina


Maonyesho yakiendelea


Waziri Membe akichukua nambari ya Mshindi katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya wa Kichina, katika bahati nasibu iliyochezeshwa katika hafla hiyo, mshindi wa zawadi kubwa kabisa katika Bahati nasibu hiyo alikabidhiwa Pikipiki. 

 Balozi Mbelwa Kairuki (wakwanza kulia) akishuudia Bahati nasibu ikichezeshwa na Waziri Membe.
Waziri Membe akiagana na Balozi Lu Youqing mara baada ya kumaliza kufungua maadhimisho ya mwaka mpya wa Kichina

Mkurugenzi Kituo cha uwekezaji Tanzania Bibi. Julieth Kairuki(Katikati), Mkurugenzi Idaya ya Habari Maelezo Bwa. Assah Mwambene (wakwanza kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga wakiwa katika picha ya pamoja

Picha na Reginald Philip

Friday, February 13, 2015

WAZIRI MEMBE APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WA KUWAIT,MALAWI,AFRIKA KUSINI NA KENYA.

Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Kuwait.
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Kuwait hapa nchini, Mhe.Jasem Ibrahim Al-Najem leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Mheshimiwa Waziri Bernard Membe akizungumza na Balozi mpya wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al-Najem leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam mara baada ya zoezi la kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kukamilika.
 Mazungumzo yakiendelea huku maofisa wa wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati (kushoto), Bi.Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali (kulia) na Bw. Thobias Makoba, Katibu wa Waziri wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo.
 
Mheshimiwa Waziri akipokea zawadi kutoka kwa balozi mpya wa Kuwait hapa nchini mara baada ya kuwasilisha Nakala ya Hati ya Utambulisho.
 Balozi mpya wa Kuwait hapa nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al-Najem akiwa katika picha ya pamoja na waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe (kulia) pamoja na Mheshimiwa Balozi Hassan Simba 
 Yahya. 

Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mpya wa Malawi
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Bernard Membe akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Malawi hapa nchini Mhe.Hawa Ndilowe leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Balozi mpya wa Malawi hapa nchini Mhe. Hawa Ndilowe akimsikiliza Mhe.Membe mara baada ya kukabidhi Nakala za Hati za Utambulisho ofisini kwa Waziri jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mpya wa Malawi hapa nchini Mhe. Hawa Ndilowe 

Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Afrika Kusini
 Balozi mpya wa Afrika Kusini hapa nchini Mhe.Thamsanqa Dennis Msekelu akiwasilisha Nalaka za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa waziri Membe akifanya mazungumzo na Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini ofisini kwake muda mfupi baada ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho.


Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi wa Kenya
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Kenya hapa nchini Mhe. Chirau Ali Mwakwere leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Kenya hapa Nchini pamoja na Naibu wake wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe baada ya kukabidhi Nakala za Hati za Utambulisho.
 Balozi wa Kenya hapa Nchini pamoja na Naibu wake wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe baada ya kukabidhi Nakala za Hati za Utambulisho,huku afisa wa wizara ya Mambo ya Nje Bi.Zulegha Tambwe akinukuu mambo muhimu katika mazungumzo hayo.

 Mheshimiwa Waziri akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Kenya hapa nchini.
===========
Picha na Reuben Mchome.