Wednesday, October 25, 2017

Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wapya kutoka nchini Oman, Uholanzi na China

Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Oman nchini, Mhe. Ali bin Abdallah bin Salim Al-Mahrooqi mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Mhe. Al-Mahrooqi.
Wakiwa katika mazungumzo ambapo maongezi yao yalijikita katika kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia sambamba na ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji ambao ndio msingi mkuu wa kuinua uchumi wa mataifa hayo.
Picha ya pamoja.  
Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin akimtambulisha Mhe. Al-Mahrooqi kwa Mhe. Rais Magufuli kabla ya kukabidhi Hati za Utambulisho.
Mhe. Al-Mahrooqi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Balozi Al-Mahroooqi akipigiwa Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Oman mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.                     
=========================================================

Wakati huohuo Mhe. Rais Magufuli alipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Uholanzi.


Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Jeroen Verheul mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin akimtambulisha Mhe. Verheul kwa Mhe. Rais Magufuli.    
Picha ya pamoja Viongozi na Maafisa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ubalozi wa Uholanzi nchini.     
Mhe. Waziri Mahiga akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mary Matari kwa Mhe. Verheul.
Mhe. Rais Magufuli akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho. 
 
Mhe. Verheul akipigia wimbo wa Taifa wa Tanzania na Uholanzi na bendi ya polisi na baadae aliagana na kiongozi wa bendi hiyo.
====================================================================
Katika nafasi nyingine Mhe. Rais Magufuli alipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa China nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho za Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke mwenye makazi yake Jijini Dar es Salaam. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Balozi Grace Martini akimtambulisha Mhe. Wang kwa Mhe. Rais Magufuli kabla ya kukabidhi Hati hizo.
Picha ya pamoja.
Mhe. Wang akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Wangi akiagana na kiongozi wa Bendi ya Polisi mara baada ya kukamilisha hafla ya makabidhiano.

Maadhimisho ya Miaka 72 ya Umoja wa Mataifa yafana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa. Maadhimisho hayo ambayo hufanyika tarehe 24 Oktoba kila mwaka yalibeba kaulimbiu isemayo "Maendeleo ya Viwanda na Utunzaji wa Mazingira kwa Maendeleo Endelevu".
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea heshima ya wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Wageni waalikwa wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa kwa ajili maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wakishuhudia upandishwaji wa Bendera ya Umoja wa Mataifa (Flag Raising) ikiwa ni ishara ya kilele cha maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza machache wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez naye akitoa salamu za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Kikundi cha Burudani cha Wanafunzi kutoka Zanzibar kikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakiimba wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez akimkabidhi tuzo maalum  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua ushirikiano na mchango wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Mahiga naye akipokea tuzo kutoka kwa Bw. Rodriguez. Kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo nchini
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.
Maafisa Mambo ya Nje ambao wameshiriki  Maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa wakiwa katika picha ya kumbukumbu
Sehemu nyingine ya Maafisa kutoka Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki  maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.
Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipata picha ya kumbukumbu wakati wa maadhimisho ya miaka 72 ya Umoja wa Mataifa






Tuesday, October 24, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa China nchini, Mhe.Wang Ke. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.


Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Mhe. Wang kwa kuteuliwa kwake kuja kuiwakilisha Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na kwa kuwa Mwakilishi wa kwanza mwanamke kutoka Taifa hilo nchini. Mhe Wange aliwasili nchini Tarehe 22 Oktoba 2017.  


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (kulia) na Mkuu wa Itifaki, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea mara baada ya makabidhiano.

Maafisa wa Ubalozi wa China nchini waliofuatana na Mhe. Wang wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Wakijadiliana jambo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi. Justa Nyange

Picha ya pamoja.

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizunguzma na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Bi. Inmi Patterson alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani. Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 24 Oktoba, 2017.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mary Matari akiwa na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Redemptor Tibaigana wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Kaimu Balozi wa Marekani (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea. Kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Marekani.

Friday, October 20, 2017

Ujumbe wa Mfalme wa Oman watembelea eneo la EPZA-Bagamoyo

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo akimtambulisha Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) kwa Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman mara baada ya kuwasili katika eneo la mradi wa Bandari ya Bagamoyo na kupokelewa na uongozi wa Mkoa wa Pwani, tarehe 19 Novemba 2017.

Ujumbe wa viongozi wa Serikali ya Tanzania ukiwa umeongozwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (wa sita kutoka kushoto) na Ujumbe wa Mfalme wa Oman wakiwa katika picha ya pamoja kwenye jiwe la msingi la Mradi huo. kutoka kulia Balozi wa Oman nchini Mhe. Ali Abdullah Al-Mahruqi, Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima.

Mhe. Ndikilo akipokea zawadi kutoka kwa Mhe. Dkt. Mohammed.

Ujumbe wa Mfalme ukipokea maelezo ya Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ambao utahusisha Maendeleo ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi (SEZ) kutoka kwa Mhe. Ndikilo, viongozi pamoja na wataalam wengine alioambatana nao. 

Mwakilishi kutoka Mfuko wa Oman ambao pia ni mbia katika Ujenzi wa Bandari hiyo akitoa maelezo kwa viongozi. Wabia wengine katika ujenzi wa mradi huo ni pamoja na  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China.

===================================
Wakati huo huo Ujumbe wa Mfalme wa Oman ulipata fursa ya kutembelea eneo la kihistoria la Kaole Wilayani Bagamoyo, ambapo waliweza kusikia mengi kuhusiana na historia ya eneo hilo na kujionea maeneo mbalimbali yanayohusisha historia ya Tanzania na Oman.
Mhe. Dkt. Mohammed akinywa Maji katika kisima ambacho maji yake huwa hayakauki na hivyo iliaminika kuwa ukinywa maji hayo unaongeza siku zako za uhai.
Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na Mhe. Dkt. Mohammed mara baada ya kumaliza ziara yake katika eneo la kihistoria la Kaole.

=======================================
Katika nafasi nyingine Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam sambamba na wanafuzi kutoka katika shule mbalimbali za Mkoa huo walipata nafasi ya kutembelea Meli ya Mfalme wa Oman "Fulk Al salaam." kama wanavyoonekana katika picha.


Mkutano na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Miaka 72 ya Umoja wa Mataifa.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Suzan Kolimba (Mb) akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari( Hawako pichani) kuhusu maadhimisho ya Miaka 72  ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC), tarehe 19 Oktoba,2017, Dar es Salaam, kulia kwake ni Bw. Alvaro Rodriguez Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini na kushoto ni Balozi Celestine Mushy Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa . Mwaka huu siku hii itaadhimishwa katika viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam Oktoba 24,2017 , Maadhimisho hayo yatafikia kilele katika tukio litakalofanyika katika Kisiwa cha Unguja, Zanzibar. Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni "Maeendeleo ya Viwanda hayana budi kuzingatia Utunzaji Mazingira ili kuleta Maendeleo endelevu".

Baadhi ya maafisa wa Wizara na Umoja wa Mataifa, wakifuatilia mkutano huo, wa kwanza kulia ni Bi. Wendy Bigham - Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Sihirika la Chakula Duniani(WFP), Bw. Jestus Nyamanga Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na mwisho ni Bw. Charles Faini Katibu wa Naibu Waziri.

Thursday, October 19, 2017

Watanzania wahimizwa kudumisha na kuuenzi utamaduni wao

Mgeni rasmi, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla (Kushoto) akikaribishwa na Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman, Mhe. Dkt. Mohammed Hamad Al Rumhy (kulia) mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki katika sherehe za utamaduni wa muziki wa Oman zilizofanyika tarehe 18 Oktoba 2017.

Kikundi cha ngoma kutoka nchini Oman ambacho ni sehemu ya ujumbe wa Mfalme wa Oman uliopo nchini kwa ziara kikitumbuiza jukwaani.

Mhe. Dkt. Kigwangalla na Mhe. Dkt.Mohammed wakijadiliana jambo.
Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima akifuatilia buruduni iliyokuwa ikitolewa na kikundi cha ngoma kutoka Oman. Wengine ni sehemu ya ujumbe wa Serikali ya Tanzania na Oman.
Sehemu nyingine ya ujumbe wa Oman ikifuatilia burudani.
Bendi ya Jeshi kutoka nchini Oman ambayo pia ni sehemu ya ujumbe huo ilitoa burudani kwa wananchi waliohudhuria hafla hiyo.


=======================================================================


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla amewataka Watanzania kuwa mabalozi wazuri katika kuzitangaza na kuzidumisha mila, tamaduni na desturi zao kwakua ndio nguzo na utambulisho wa Mtanzania popote Duniani.

Waziri Kigwangala aliyasema hayo katika sherehe za muziki wa utamaduni wa Oman zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Oktoba 2017.

Sherehe hizo ambazo Mgeni rasmi alikuwa Mhe. Dkt. Kigwangalla, ziliandaliwa na ujumbe wa Mfalme wa Oman uliokuja na Meli ya Mfalme huyo nchini kwa ziara ya siku sita inayotarajiwa kumalizika siku ya Jumamosi tarehe 21 November 2017.

Mhe. Kigwangala alisema kupitia tamasha hilo la muziki na ziara nzima kwa ujumla, Oman inapata fursa ya kujitangaza na kuutumia utamaduni wao  kama sehemu ya utalii na kwamba hii ni nafasi ya pekee kwa Watanzania kujifunza namna gani watu wa mataifa mengine wameweza kutumia utamaduni wao kwa tija na kuongeza pato la Taifa. 

Aidha, alisisitiza ni wakati sasa makundi yote ya utalii  yaliyopo nchini kama utalii wa kwenye maji, utalii wa misitu hususan kwa kutumia upekee wa mazingira yetu, fukwe na hata historia ya binadamu vikaendelea kuhifadhiwa na kupatiwa ubunifu zaidi wa namna ya kuvitangaza na kupata mfumo wa kisasa kwa ajili ya kuwezesha watalii wengi kuingia na kutoka nchini kwa namna bora zaidi.

Halikadhalika akaongeza kwa kusema “Nchi yetu imebarikiwa sana kwa kuwa na idadi kubwa ya vivutio vya utalii ukilinganisha na Oman, katika fursa niliyopata ya kukutana na Naibu Waziri wa Utalii wa Oman ambaye ameambatana na ujumbe huu nimeweza kuzungumza naye mengi ambayo tutayaweka katika utekelezaji ili sekta ya utalii iweze kuongeza fedha za kigeni zaidi.”

Kwa upande wake Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman Bw. Mohammed bin Hamad Al-Rumhy ameahidi kuwa Serikali ya Oman itaendeleza undugu huo kwa kufanya biashara  na kuongeza uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuweza kuingia katika soko la ushindani duniani.

Lengo kuu la ziara ya ujumbe huo ni kutangaza amani katika ukanda wa Afrika Mashariki sambamba na kudumisha undugu uliopo baina ya Tanzania na Oman ambapo utamaduni wa mataifa haya mawili umekuwa ukifanana hususan katika ukanda wa pwani kufuatia historia na muingiliano wa wananchi wake katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.