Thursday, February 7, 2019

Wabunge wa EALA walivyotoa Elimu ya Mtangamano wa EAC

Mkurugenzi Mkazi wa Trade Mark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga akitoa mada kwa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kuhusu shghuli za taasisi hiyo. Alisema taasisi yake inashirikiana na Serikali kuboresha miundombinu mbalimbali kwa madhumuni ya kuhakikisha kuwa biashara katika nchi za EAC inafanyika bila vikwazo.

Waheshimiwa Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakijadili kwa pamoja na Mkurugenzi wa TMEA kuhusu mchango wa taasisi hiyo katika kuboresha mwenendo wa biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine za EAC.

Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakijadili mada iliyowasilishwa na Mkurugenzi Mkazi wa TMEA.

Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam

Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la EALA, Mhe. Dkt. Abdallah Makame (kulia) akijadili jambo na Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar Es Salaam mara baada ya kuwasili katika chuo hicho kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu EAC. 

Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la EALA, Mhe. Dkt. Abdallah Makame (kulia) akipata chakula cha mchana na wanafunzi wa UDSM katika Cafteria Namba moja ya Chuo hicho. Mwenye nguo za bluu ni Mbunge mwenzake wa EALA, Mhe. Pamela Maasay.

Wanafunzi wa UDSM wakipata chakula cha mchana ambapo Wabunge wa EALA walijumuika nao katika chakula hicho.

Mbunge wa EALA, Mwalimu Josephine Sabastian (kushoto) akibadilishana mawazo na wanafunzi wa UDSM wakati wakipata kwa pamoja chakula cha mchana Cafteria.
Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakiwa katika meza kuu kwenye Ukumbi wa Nkurumah kwa ajili ya kuongea na wanafunzi kuhusu fursa za EAC.
Mbunge wa EALA, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe akiwasilisha mada kuhusu EAC kwa wanafunzi wa UDSM.

Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakiongea na wanafunzi wa UDSM kuhusu fursa za Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Wanafunzi walioshiriki kwenye mazungumzo na Wabunge wa EALA. Mwenye suti ya bluu ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam.
Washiriki wengine katika mazungumzo hayo.


Wanafunzi wakiuliza maswali na kutoa maoni namna Watanzania watakavyofaidika na Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki



Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakikabidhi bendera ya EAC kwa viongozi wa UDSM ili iwe inapeperushwa chuoni hapo. Walitoa wito kwa taasisi nyingine, hususan za Serikali kupeperusha bendera hiyo.
Mkutano na Asasi za Kiraia
Mbunge wa EALA, Mwalimu Josephine Sabastian akitoa elimu kuhusu EAC kwa wawakilishi wa Asasi za Kiraia zilizopo hapa nchini.



Majadiliano baina ya Wabunge wa EALA na wawakilishi wa Asasi za Kiraia kuhusu ushiriki wa asasi hizo katika masuala ya EAC.

Wabunge wa EALA na wawakilishi wa Asasi za Kiraia wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wabunge walisisitiza umuhimu wa wimbo huo kupigwa katika shughuli rasmi za Serikali.
Mdau akifanya tafrisi ya lugha ya ishara kwa watu wenye ulemavu wa kusikia.

Wednesday, February 6, 2019

Vacancy announcement




PRESS RELEASE

Job Announcement at the Commonwealth Secretariat

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received vacancy notification from the Commonwealth Secretariat inviting qualified Tanzanians to apply for the post of Business Analyst available at the Commonwealth Secretariat.

In line with the Comonwealth’s commitment to gender equality, the Commonwealth Secretariat encourages applications from appropriately qualified women for this post.

Application details can be found on the Secretariat’s website, http://thecommonwealth.org/jobs. Closing date for application is Sunday 17th February, 2019.

Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
6th February, 2019.

Tuesday, February 5, 2019

Jengo la Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje lasonga kwa kasi Dodoma


Mafundi wakiwa katika harakati kuhakikisha kuwa jengo linamalizika kwa wakati.

Linapendeza kweli kweli.

Palasta inaendelea kupigwa.

Kumenoga, tazama mwenyewe.

Kazi nje na ndani. Usiku na mchana. Mtumba Oyeeeee.

Monday, February 4, 2019

Wabunge wa EALA watoa elimu ya Mtangamano wa EAC

Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Abdallah Makame na Katibu wake, Mhe. Josephene Sabastian wakiwa katika kikao na Wabunge wenzao wa Tanzania, maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bunge la EALA na Trade Mark East Africa katika Hoteli ya Serena. Mkutano huo ni maandalizi ya zoezi la siku nne la kutoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu fursa za Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuanzia tarehe 04 hadi 07 Februari 2019 jijini Dar Es Salaam. 

Mhe. Habib Mnyaa, Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mhe. Maryam Ussi wakishiriki kikao cha maandalizi ya zoezi la kutoa elimu kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe. Pamela Maasay (kulia) na Mhe. Happiness Legiko wakijiandaa kukutana na wadau mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu ya Mtangamano.

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambao Wizara yao ndio mratibu w masuala ya Mtangamano wakiwa katika kikao cha maandalizi cha kutoa elimu ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Maafisa kutoka Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika kikao cha maandalizi ya zoezi la kutoa elimu kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe. Dkt. Abdallah Makame akitoa maelekezo kwa Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa dawati la Bunge.

Kikao kinaendelea

Mkutano wa Waandishi wa Habari

Waheshimiwa Wabunge wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari kuwaeleza zoezi walilopanga la kuelimisha wadau kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Waandishi wamefurika kusikiliza Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu zoezi la kuelimisha wadau kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Waheshimiwa wabunge (kushoto) na waandishi wa habari wkiendelea na mkutano wao.

Bandari ya Dar Es Salam 
Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar Es Salaam akiwakaribisha Wabunge wa EALA katika Bandari ya Dar Es Salaam. Waheshimiwa Wabunge walienda Bandari ya Dar Es Salaam kuona maboresho yanayofanywa na bandari hiyo pamoja na kusikiliza wadau wanotumia bandari hiyo changamoto wanazokutana nazo.

Waheshimiwa Wabunge walienda kutembelea gati namba moja ambalo ni moja ya mageti ynayofnyiwa maboresho makubwa.

Siku ya Kuzaliwa
Mheshimiwa Maryam akisherehekea Siku yake ya kuzaliwa tarehe 04 Februari kwa kuwalisha keki Wabunge wenzake.

Happy Birthday kwa Mhe. Maryam Ussi kutoka kwa Mhe. Fancy Nkuhi.

Friday, February 1, 2019

Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa EAC wamalizika Arusha

Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wakiwa wamesimama kutoa heshima wakati wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ukiimbwa kabla ya kuanza rasmi Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutsno cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 1 Februari 2019. Katika picha ni Mhe. Yoweri Kaguta Museveni (wa nne kulia), Rais wa Uganda, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (wa tatu kulia), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Paul Kagame (wa nne kushoto), Rais wa Rwanda, Mhe. Uhuru Kenyatta (wa tatu kushoto), Rais wa Kenya, Mhe. Gaston Sindimo (wa pili kulia), Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi ambaye alimwakilisha Rais wa nchi hiyo Mhe. Pierre Nkurunziza, Mhe. Paul Mayom Akechi (wa pili kushoto), Waziri wa Biashara, Viwanda na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Sudan Kusini ambaye alimwakilisha Rais wa nchi hiyo Mhe. Salva Kiir. Wengine katika picha ni Mhe. Kirunda Kivejinja (kulia), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Uganda ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo na Dkt. Liberat Mfumukeko (kushoto), Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pamoja na mambo mengine, Mhe. Paul Kagame, Rais wa Rwanda alikabidhiwa uenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja na Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ambaye amemaliza muda wake. Pia Wakuu hao walishuhudia kuapishwa kwa Jaji mpya wa Mahakama ya Haki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Jaji Sauda Mjasiri kutoka Tanzania.
Marais wanne walioshiriki Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kama wanavyonekana kwenye picha. Kutoka kulia ni Mhe. Dkt. Magufuli, Mhe. Rais Museveni, Mhe. Rais Kagame na Mhe. Rais Uhuru
Mkutano ukiendelea









Thursday, January 31, 2019

Kampuni ya Kenya kununua tani laki moja za korosho Tanzania


Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, Dkt. Hussein Mansoor (kushoto) kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya INDO Power Solutions ya nchini Kenya, Bw. Brian Mutembei (kulia) wakisaini Mkataba wa mauziano ya korosho ghafi kiasi cha tani laki moja kwa malipo ya Shilingii bilioni 418. Wanaoshuhudia tukio hilo muhimu ni Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (wa pili kushoto), Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Joseph Kakunda (kushoto), Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Innocent Bashungwa (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Kilimo na Mhe. Dan Kazungu, Balozi wa Jamhuri ya Kenya nchini. Tukio hilo lilifanyika kwenye Ukumbi wa mikutano uliopo Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha tarehe 30 januari 2019. Mawaziri hao wapo jijini humo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. Mansoor na Bw. Mutembei wakibadilishana Mkataba huo mara baada ya kusaini
Mhe. Prof. Kabudi akizungumza kabla ya kuanza kwa tukio hilo la kihistoria la kusainiwa mkataba wa ununuzi wa tani laki moja za korosho ghafi
Mhe. Kakunda nae akizungumza

Mhe. Dkt. Bashungwa akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)
Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Kazungu akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi ya kusainiwa mkataba wa ununuzi wa tani laki moja za korosho kutoka Tanzania
Bw. Mutembei nae akieleza furaha yake katika kukamilisha ununuzi wa korosho kutoka Tanzania
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Joseph Buchweshaija akizungumza kwa ufupi kuhusu hafla hiyo ya uwekaji saini mkataba wa ununuzi wa korosho. Wengine katika picha ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Mhe. Prof. Florens Luoga ( kulia walioketi) akifuatiwa na Prof. Sifuni Mchome, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria na Dkt. Evaristo Longopa, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Mkutano ukiendelea. Kushoto ni Mkurugenzi wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka
=============================================================================================


Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Taifa ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko imesaini mkataba wa mauzo ya korosho ghafi kiasi cha tani laki moja kwa Kampuni ya Kenya ya INDO Power Solutions kwa malipo ya Shilingi bilioni 418.

Mkataba huo umesainiwa jijini Arusha tarehe 30 Januari 2019 kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Dkt. Hussein Mansoor kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw. Brian Mutembei, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya INDO Power Solutions ya nchini Kenya.

Tukio hilo la kihistoria lilishuhudiwa na Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Joseph Kakunda, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Innocent Bashungwa, Naibu Waziri wa Kilimo, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga,  Dkt. Evaristo Longopa, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali,

Viongozi wengine walioshuhudia ni Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dan Kazungu, Prof. Sifuni Mchome, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Prof. Joseph Buchweshaija, Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Prof. Siza Tumbo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Edwin Rutaberuka, Mkurugenzi wa TanTrade, Maafisa Waandamizi kutoka Serikalini na Waandishi wa Habari.

Awali wakizungumza kabla ya kusainiwa kwa Mkataba huo Mawaziri hao wakiongozwa na Prof. Kabudi, kwa pamoja walipongeza kwa dhati uamuzi wa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Serikali kununua korosho kutoka kwa wakulima ili kuepusha wakulima hao kuuza korosho zao kwa bei ya chini kwa watu wasio kuwa na nia njema kwa wakulima. Itakumbukwa kuwa, mwezi Novemba 2018, Mhe. Rais Magufuli alitoa maelekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo waratibu zoezi  la ununuzi wa korosho kutoka kwa wakulima kwa shilingi 3,300 kwa kilo moja.

Kwa upande wake Prof. Kabudi alisema kuwa anampongeza  Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi huo wa Serikali kununua korosho yote ili wakulima wapate bei inayolingana na jasho lao ambao hatimaye umezaa matunda kwa faida na maendeleo ya nchi.

Naye Mhe. Kakunda alieleza kuwa Bw. Mutembei ni mnunuzi wa kwanza kati ya wengi ambao walikuwa kwenye mazungumzo na Serikali kuhusu ununuzi wa korosho hizo. Mhe. Kakunda alisema katika majadiliano Serikali iliangalia kufanya biashara ya faida ambayo itawezehsa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo gharama za upakiaji na upakuaji, malipo kwenye Serikali za Mtaa na michango mingine ya kijamii kwa mujibu wa makubaliano. Hivyo aliwataka watanzania na wenye viwanda kutokuwa na wasiwasi kwani Serikali ina nia njema ya kuwaletea maendeleo wananchi hususan kupitia sekta ya kilimo cha korosho.

“Wakulima wa Korosho wanatakiwa kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi wake ambao unalinda maslahi ya mkulima na umewawezesha kuuza korosho zao kwa faida. Nawakaribisha wafanyabiasha makini kuja nchini kwani Serikali ipo tayari kuwasikiliza watu wa aina hiyo na kufanya nao biashara” alisema Mhe. Kakunda.

Kwa upande wake, Mhe. Bashungwa alieleza kuwa katika msimu wa korosho wa mwaka 2018/2019 tayari zimekusanywa tani 213,159 ambazo kati ya hizo tani 126,194 zimehakikiwa na tayari  wakulima wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Pwani wamelipwa fedha zao kwa zaidi ya asilimia 95.5. Mhe. Bashungwa aliongeza kuwa, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha Wakulima wote kulipwa fedha zao hadi kufikia tarehe 05 Februari 2019.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Kazungu alisema kuwa kusainiwa kwa mkataba huo ni faraja kubwa kwake katika historia ya mahusiano kati ya Tanzania na Kenya ambayo yanaendelea kuimarika siku hadi siku. Aidha, alieleza kuwa mkataba huo ni mfano mzuri wa kuimarika kwa mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hususan katika masuala ya kilimo na biashara.

Kwa upande wake, mnunuzi wa korosho hizo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Indo Power Solutions, Bw. Mutembei alisema amekuja kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Magufuli za kumwinua mkulima wa Tanzania na kwamba anawataka wale wote wanaobeza jitihada hizo za Mhe. Rais Magufuli kuacha mara moja huku akilaani kitendo cha baadhi ya wafanyabiashara kuendelea kuwakandamiza wakulima kwa kununua mazao yao kwa bei ndogo wanazopanga wao huku wakijua wazi kuwa wakulima hao wametumia gharama kubwa katika uzalishaji wa mazao hayo.

Pia aliwataka wafanyabiashara kufuata taratibu na sheria katika kufanya biashara kama Serikali zinavyoelekeza na kuacha kuchanganya biashara na siasa.

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka, Dkt. Mansoor alieleza kufurahishwa na tukio hilo ambalo limekuja wakati mwafaka wakati nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zikijiandaa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika jijini humo hivi karibuni. Aidha alisema kuwa, kwa kiasi kikubwa tukio hilo limeiinua Bodi yake na kwamba anatoa wito kwa wafanyabiasha wengine wa ndani na nje ya Tanzania kuja nchini na kushirikiana na Bodi hiyo ili kuwakomboa wakulima wengi Zaidi.

Mkataba huo umesainiwa wakati baadhi ya Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Tanzania wakiwa jijini Arusha kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 1 Februari 2019.