Sunday, October 8, 2023

MTENDAJI MKUU WA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA KAOLE- BAGAMOYO



Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi akiangalia mabaki ya vitu mbalimbali vilivyohifadhiwa katika  Makumbusho ya Kaole mjini Bagamoyo Mkoani Pwani alipotembelea kujionea historia ya mabaki ya mawe ya zamani, magofu na vitu vingi vya kale yakiwemo makaburikatika makumbusho hiyo


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal Al-Moosawi akiangalia mabaki ya vitu mbalimbali vilivyohifadhiwa katika makumbusho ya Kaole mjini Bagamoyo


Mhifadhi wa makumbusho katika Makulbusho ya Kaole mjini Bagamoyo akimuelezea Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal Al-Moosawi historia ya vitu vivyohifadhiwa katika Makumbusho hiyo


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia gofu lenye mnara mrefu alipotembelea Makumbusho ya Kaole mjini Bagamoyo


Balozi wa Oman nchini Mhe. Saud bin Hilal Alshaidani akisoma  historia ya watu na mabaki ya vitu mbalimbali vilivyohifadhiwa katika Makumbusho ya Kaole mjini Bagamoyo alipotembelea makumbusho hiyo

Balozi wa oman nchini Mhe. Saud bin Hilal Alshaidani akinawa maji maarufu yanayopatikana katika kisima kinachoaminika kuchimbwa katika karne ya 13 mjini Bagamoyo katika Makumbusho ya Kaole  alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia Kisima cha maji maarufu yanayopatikana katika kisima kinachoaminika kuchimbwa na kutumika katika karne ya 13 mjini Bagamoyo katika Makumbusho ya Kaole  alipotembelea makumbusho hiyo


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akinawa maji ya kisima maarufu ya kaole alipotembelea makumbusho hayo
Mmoja wa wageni kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman akinawa maji maarufu yanayopatikana katika makumbusho ya kaole mjini Bagamoyo walipotembelea makumbusho hayo mjini Bagamoyo mkoani Pwani

 

Ujumbe wa Makumbusho ya Taifa ya Oman ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi umetembelea Makumbusho ya Kaole yaliyoko Bagamoyo Mkoani Pwani na kujionea mabaki ya mawe ya zamani, magofu na vitu vingi vya kale yakiwemo makaburiambayo ni sehemu ya historia ya kale vilivyotumiwa na Waarabu katika karne ya 13 mpaka karne ya 16.
 

Ujumbe huo kutoka Oman ambao uko nchini kukutana na wenzao wa Makumbusho ya Taifa kwa ajili ya kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Oman ulihudhuria Mkutano wa Kwanza wa Pamoja wa Wataalamu kati ya Makumbusho ya Taifa ya Tanzania na Makumbusho ya Taifa ya Oman.
 

Ujumbe huo uliambatana na Balozi wa Oman nchini Tanzania Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga.

Ujumbe huo kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman unatarajia kwenda katika Visiwa vya Zanzibar ambako utatembelea Mji Mkongwe, Makumbusho ya amani na historia ya Mnazi Mmoja, Jumba la Kibweni na Magofu ya Mtoni. 

Ujumbe huo pia utatembelea Pango la Kuumbi la Jambiani na Makumbusho ya Unguja Kuu kwa ajili ya kujifunza na kujionea historia ya Zanzibar. 


Ujumbe huo kutoka nchini Oman uliwasili nchini tarehe 05 Oktoba, 2023 unatarajiwa kuondoka nchini tarehe 12 Oktoba 2023 kupitia Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

UJUMBE WA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN WATEMBELEA MAKUMBUSHO YA KUNDUCHI

 

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi akisini kitabu cha wageni alipowasili katika  Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salam, kulia ni Balozi wa Oman nchini Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akitembelea magofu ya Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi na ujumbe wake wakiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam walipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi na ujumbe wake wakiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam walipotembelea makumbusho hiyo



Ujumbe wa Makumbusho ya Taifa ya Oman ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi umetembelea Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salam.


Katika Makumbusho hiyo yamehifadhiwa magofu ya Kale ambayo ni Makaburi ya masultani waliozikwa na binti vigori wakiwa hai ili kumsindikiza sultan katika safari yake hiyo ya kaburini na Msikiti uliotumika tangu karne ya 15.


Ujumbe huo kutoka Oman ambao uko nchini uliambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima na Balozi wa Oman nchini Tanzania Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani.


Ujumbe huo pia uliambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga.

UJUMBE WA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN WATEMBELEA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO

Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo (wa Kwanza kushoto),  Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima (wa pili kushoto) na Balozi wa Oman nchini Mhe. Saud bin Hilal Alshaidani walipotembelea kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam 

 

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisaini kitabu cha Kumbukumbu ya wageni katika Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdallah Kilima na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo walipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam.


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akipanda mti alipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiwa ndani ya nyumba iliyohifadhiwa katika  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa makumbusho alipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia ngoma ya utamaduni alipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa makumbusho alipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi katika picha ya pamoja na ujumbe wake walipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam



Ujumbe kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho hiyo Mheshimiwa Jamal al-Moosawi umetembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujifunza na kujionea historia, mila na tamaduni za makabila mbalimbali ya Tanzania. 

 
Ujumbe huo kutoka nchini Oman ambao uko nchini umeambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima na Balozi wa Oman nchini Tanzania Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani.
Ujumbe huo pia uliambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga.

 
Akiongea baaada ya kutembelea Kijiji cha Makumbusho Mhe. Al Moosawi alielezea kuridhishwa kwake na uhifadhi wa historia ya makabila ya Tanzania ambayo ameisikia na kuona jinsi nyumba za makabila hayo kama zilivyooneshwa katika eneo hilo na kupongeza jitihada za kuhifadhi historia hiyo kwa ajili ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Kijiji cha makumbusho ni eneo linalohifadhi mifano ya nyumba na vifaa vya makabila na tamaduni mbalimbali zinazopatikana Tanzania.
Eneo hilo lilianzishwa mwaka 1966 kwa ajili ya kuonyesha na kutunza tamaduni za asili, ngoma na tamaduni za makabila mbalimbali kama Wanyakyusa, Wamakonde, Wamasai, Wachagga, Wahaya, Wangoni, Wayao na mengine mengi.

 

PRESS STATEMENT


 

Saturday, October 7, 2023

WAZIRI MAKAMBA ATUA INDIA KUELEKEA ZIARA YA KIHISTORIA YA MHE. RAIS DKT. SAMIA NCHINI HUMO










 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. January Makamba amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Dkt.Subrahmanyam Jaishankar ikiwa ni maandalizi ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan atakayoifanya nchini humo kuanzia  tarehe 8 hadi 11 Oktoba 2023.



Katika mazungumzo yao yaliyofanyika hivi karibuni jijini New Delhi, viongozi hao pamoja na mambo mengine wamelezea matarajio yao ya kuimarika zaidi kwa ushirikiano kati ya Tanzania na India kupitia ziara hiyo ya kihistoria.



Kwa upande wake , Mhe. Makamba amemshukuru mwenyeji wake kwa kumkaribisha nchini humo lakini pia kwa maandalizi mazuri ya ziara ya Mhe.  Rais Dkt. Samia nchini humo.



Kadhalika, Mawaziri hao walibadilishana taarifa kuhusu ushirikiano uliopo baina ya nchi hizi mbili na kukubaliana kuongeza jitihada ili kufikia malengo ya pamoja ya kuinua kuwango cha biashara na uwekezaji kati ya nchi hizi mbili na kuhakikisha ushirikiano uliopo unazaa matokeo tarajiwa.



Mhe. Rais Dkt. Samia anatarajiwa kuwasili India tarehe 8 Oktoba 2023 kwa ziara ya kitaifa ya siku tatu.



Wakati  wa ziara hiyo kutashuhudiwa ubadilishanaji wa mikataba  mbalimbali ya ushirikiano katika sekta za uwekezaji, uchukuzi,  afya, maji na nyingine nyingi.



Ziara hiyo pamoja  na mambo mengine inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na India hususan  kwenye maeneo ya kimkakati  na manufaa kwa Tanzania ikiwemo afya, maji, elimu uchumi wa buluu,  teknolojia, kilimo, na biashara na uwekezaji. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. January Makamba akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Dkt.Subrahmanyam Jaishankar ikiwa ni maandalizi ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan atakayoifanya nchini humo kuanzia  tarehe 8 hadi 11 Oktoba 2023. Mazungumzo yao yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya India jijini New Delhi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akizunguza na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe.Binaya Srikanta Pradhan jijini New Delhi kabla ya Mhe. Makamba kukutana na Waziri wa mambo ya Nje wa India, Mhe. Dkt. Jaishankar
Mhe. Waziri Makamba akimsikiliza Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega wakati wa kikao cha kupokea taarifa kuhusu ushirikiano wa Tanzania na India mara baada ya Mhe. Makamba kuwasili nchini India tarehe 6 Oktoba 2023 kwa ajili ya kutathmini na kukamilisha maandalizi ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini humo kuanzia tarehe 8 hadi 1 Oktoba 2023
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega (kulia) akiwa na Mkrugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga (kushoto) wakati wa kikao na Mhe. Waziri Makamba (hayupo pichani) baada ya kuwasili nchini India. Wengine katika picha ni Mkuu wa utawala Ubalozini, Bw. Deogratius Dotto na Afisa Mwandamizi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania, Bi. Latifah

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. John Kambona (kulia) akiwa na Afisa Mwandamizi wa Idara hiyo Bi. Eliet Magogo na Katibu wa Mhe. Waziri Makamba, Bw. Seif Kamtunda wakati wa kikao cha ujumbe wa Tanzania na Mhe. Waziir Makamba (hayupo pichani) jijini New Delhi kuelekea ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini India tarehe 8 hadi 11 Oktoba 2023
Mhe. Makamba akizungumza na Mkurugenzi wa masuala ya ushirikiano wa India na Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya India mara baada ya kuwasili nchini humo kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya ziara ya Mhe. Rais Dkt. Samia. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega

Picha ya pamoja













 

Friday, October 6, 2023

MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN WATEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA TANZANIA

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi (kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mtalamu wa Makumbusho alipotembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam
Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi (kushoto) akiangalia kitabu kilichowekwa mezani na mtaalamu wa Makumbusho alipotembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam

 



Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi (aliyeshika koti) akizungumza kitu alipotembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam

 

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi (mwenye tai) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Luoga alipotembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam
Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi (kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mtalamu wa Makumbusho alipotembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam

 

 

 

 

Ujumbe wa watu sita kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman umetembelea Makumbusho ya Taifa Dar es Salam kwa ajili ya kujifunza na kujionea historia ya Tanzania.

Ujumbe huo unaongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi.  Pamoja na mambo mengine, ujumbe huo unatarajia pia kutembelea Kijiji cha Makumbusho  Kijitonyama, Jumba la Atiman na Jengo la Boma la zamani yaliyoko katika Mtaa wa Sokoine ambapo majengo hayo yaliyojengwa na kukaliwa na Sultan wa Zanzibar miaka ya 1860’s.

Ujumbe huo kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman unatarajia kutembelea visiwa vya Zanzibar ambapo watakutana na kuzungumza na uongozi wa watendaji wa Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale iliyochini ya Wizara ya Utalii na Urithi Zanzibar.

Ukiwa Zanzibar Ujumbe huo utatembelea Mji Mkongwe, Makumbusho ya amani na historia ya Mnazi Mmoja, Jumba la Kibweni na Magofu ya Mtoni. Ujumbe huo pia utatembelea Pango la Kuumbi la Jambiani, Makumbusho ya Unguja Kuu na  Mji Mkongwe kwa ajili ya kujifunza na kujionea historia iliyosheheni ya Zanzibar.

Ujumbe huo kutoka nchini Oman uliwasili nchini tarehe 05 Oktoba, 2023 ambapo pamoja na mambo mengine, una shiriki Mkutano wa Kwanza wa Pamoja wa Wataalamu kati ya Tanzania na Oman unaofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo unalenga kuendeleza uhusiano kati ya Tanzania na Oman kupitia Makumbusho ya Taifa ya Tanzania na Makumbusho ya Taifa ya Oman.

Mkutano huo wa Kwanza wa Pamoja wa Wataalamu kati ya Makumbusho ya Taifa ya Tanzania na Makumbusho ya Taifa ya Oman ni moja ya mbinu na nyenzo za kuimarisha Uhusiano kati ya Tanzania na Oman.

Kufanyika kwa Mkutano huo ni utekelezaji wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii na Makumbusho ya Taifa ya Oman mwezi Juni ,2022.

Ujumbe huo unatarajiwa kuondoka nchini tarehe 12 Oktoba 2023 kupitia Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.






Thursday, October 5, 2023

RAIS SAMIA KUZURU INDIA TAREHE 8-11 OKTOBA 2023