Sunday, October 8, 2023

UJUMBE WA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN WATEMBELEA MAKUMBUSHO YA KUNDUCHI

 

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi akisini kitabu cha wageni alipowasili katika  Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salam, kulia ni Balozi wa Oman nchini Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akitembelea magofu ya Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi na ujumbe wake wakiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam walipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi na ujumbe wake wakiangalia mabaki ya magofu yanayopatikana katika Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salaam walipotembelea makumbusho hiyo



Ujumbe wa Makumbusho ya Taifa ya Oman ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mheshimiwa Jamal al-Moosawi umetembelea Makumbusho ya Kunduchi jijini Dar es Salam.


Katika Makumbusho hiyo yamehifadhiwa magofu ya Kale ambayo ni Makaburi ya masultani waliozikwa na binti vigori wakiwa hai ili kumsindikiza sultan katika safari yake hiyo ya kaburini na Msikiti uliotumika tangu karne ya 15.


Ujumbe huo kutoka Oman ambao uko nchini uliambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima na Balozi wa Oman nchini Tanzania Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani.


Ujumbe huo pia uliambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.