Monday, October 30, 2023

BALOZI NJALIKAI AKUTANA NA BALOZI WA KWANZA WA ALGERIA NCHINI TANZANIA

 





Balozi wa Tanzania Nchini Algeria Mhe. Iman Njalikai amekutana na kuzungumza na Rais wa Taasisi ya Kimataifa ya Marafiki wa Algeria tangu kipindi cha Ukombozi ambaye alikuwa Balozi wa Kwanza wa Algeria nchini Tanzania Mhe. Noureddine DJoudi .

Mazungumzo na Balozi huyo mwenye historia na kumbukumbu kubwa ya uhusiano wa Algeria na Tanzania yalifanyika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Algiers.

Mheshimiwa Balozi Joudi alifika Ubalozini kufuatia mwaliko wa Balozi Njalikai kwa lengo la kufahamiana na kumpongeza kwa majukumu mapya aliyokabidhiwa na Serikali ya Algeria.

Katika mazungumzo yao Balozi Njalikai alimshukuru Balozi Joudi kwa kuendelea kuwa kiungo muhimu katika kuimarisha uhusiano kati ya Ubalozi na Mamlaka mbalimbali za Algeria ikiwemo sekta binafsi.


Mhe. Balozi Joudi ameuomba Ubalozi kuimarisha kituo cha Kiswahili kilichopo Ubalozini hapo kwa lengo la kuitangaza Lugha hiyo na kuifundisha kwa Wa' Algeria wengi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.