Saturday, October 28, 2023

KAMATI YA BUNGE YA NUU YATEMBELEA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU ARUSHA

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa walipowasili katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akiwa na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud walipokutana katika ofisi za Mahakama hiyo jijini Arusha

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato  akizungumza kitu alipokutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud (katikati) kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa walipotembelea Mahakama hiyo jijini Arusha


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa (kushoto) akizungumza na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud walipowasili katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akizungumza na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa AICC walipowasili katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha



Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakiwa na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud walipotembelea Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akiwa na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Iman Aboud na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato  na wajumbe wengine wa Kamati hiyo katika picha ya pamoja na watendaji wengine wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha



 
 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama imetembelea Mahakama ya Afrika ya Haki za  Binadamu na Watu (AFCHPR) yenye makao yako jijini Arusha na kuzungumza na Rais wa Mahakama hiyo Mhe. Jaji Iman Aboud.
 
Kamati ya NUU pia imetembelea Eneo la Lakilaki jijini Arusha ambako Serikali ya Tanzania inajenga  Mahakama hiyo ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AFCHPR)
 
Kamati imeipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuigawia  Mahakama hiyo eneo la Lakilaki na kwa kutimiza ahadi ya kujenga Mahakama hiyo.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.