Tuesday, October 10, 2023

RAIS DKT. SAMIA AKARIBISHA WAWEKEZAJI KUTOKA INDIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan amefungua rasmi Jukwaa la Uwekezaji kati ya Tanzania na India lililofanyika jijini New Delhi tarehe 10 Oktoba 2023.



Akifungua Kongamano hilo lenye kaulimbiu isemayo “Strong, Togerher ," Mhe. Rais Dkt. Samia amewakaribisha wawekezaji wa India kuja nchini  kuwekeza kwenye sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, afya, Tehama,  Utalii na Miundombinu na kuwahakikishia mazingira mazuri ya uwekezaji na ufanyaji biashara.



Amesema Tanzania imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na ufanyaji biashara kwa kurekebisha  baadhi ya sheria za usimamizi wa biashara, kuboresha huduma na miundombinu,  teknolojia pamoja na kuishirikisha kikamilifu  sekta binafsi.

 

Ameongeza kuwa kutokana na jitihada hizo,  viwango vya biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na India  vimeongezeka mwaka ha ambapo kwa takwimu za  Tanzania za mwaka 2021/2022 India  ni miongoni mwa nchi tano zinazoongoza kwa uwekezaji nchini kwa kuwekeza miradi 630 yenye thamani ya Dola za Marekani 3.7 ambayo imetengeneza ajira kwa watanzania 60,000.



Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara wa India Mhe.  Shri Piyush Goyal amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali  ya Tanzania katika kuboresha mazingira yabuwekezaji na kwamba ziara ya Mhe. Dkt. Samia inafungua ukurasa mpya wa ushirikiano kwenye sekta muhimu ikiwemo biashara na uwekezaji.



Awali akizungumza kwenye kongamano hilo Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, Bi. Angelina Ngalula amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali hizi mbili katika kuboresha mazingira ya uwekezaji  na biashara.



Amesema kutokana na jitihada hizo jukwaa hilo limehudhuriwa na zaidi ya  wafanyabiashara na wawekezaji 250 kutoka  Tanzania na India ambapo kati yao 80 wanatoka Tanzania katika sekta za   Benki, Uchukuzi, Uzalishaji viwandani, TEHAMA,   Burudani na Ubunifu wa mitindo.



Kongamano hilo ambalo limebeba mada isemayo " Nafasi ya Sekta Binafsi katika kuimarisha Biashara kati ya Tanzanaia na India litahitimishwa kwa kupitisha Azimio na Mapendekezo mbalimbali yanayolenga kuboresha sekta ya biashara na uwekezaji kati ya nchi hizi mbili. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan akifungua rasmi Jukwaa la Uwekezaji kati ya Tanzania na India lililofanyika jijini New Delhi tarehe 10 Oktoba 2023.Mhe. Rais yupo nchini India kwa zara ya kitaifa ya siku tatu

Mhe. Rais Dkt. Smia akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akimweleza jambo wakati wa Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na India lililofanyika India hivi karibuni
Sehemu ya wawekezaji kutoka Inida pamoja  jumbe wa Tanzania wakifuatilia Mkutano wa Jukwaa la Uwekezaji kati ya Tanzania na India
Mkutano wa Jukwaa la Uwekezaji kati ya Tanzania na India ukiendelea

Mhe. Rais Dkt. Samia akishuhudia ubadlishanaji wa Hati za Makubaliano ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India kwenye sekta ya uwekezaji

Mhe. Rais Dkt. Samia akishuhudia ubadlishanaji wa Hati za Makubaliano ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India kwenye sekta ya biashara
















No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.