Sunday, October 8, 2023

UJUMBE WA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA OMAN WATEMBELEA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO

Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo (wa Kwanza kushoto),  Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima (wa pili kushoto) na Balozi wa Oman nchini Mhe. Saud bin Hilal Alshaidani walipotembelea kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam 

 

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisaini kitabu cha Kumbukumbu ya wageni katika Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdallah Kilima na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo walipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam.


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akipanda mti alipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiwa ndani ya nyumba iliyohifadhiwa katika  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam alipotembelea makumbusho hiyo

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa makumbusho alipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akiangalia ngoma ya utamaduni alipotembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam

Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa makumbusho alipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam


Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Taifa ya Oman Mhe. Jamal al-Moosawi katika picha ya pamoja na ujumbe wake walipotembelea  Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam



Ujumbe kutoka Makumbusho ya Taifa ya Oman ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Makumbusho hiyo Mheshimiwa Jamal al-Moosawi umetembelea Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujifunza na kujionea historia, mila na tamaduni za makabila mbalimbali ya Tanzania. 

 
Ujumbe huo kutoka nchini Oman ambao uko nchini umeambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdallah Kilima na Balozi wa Oman nchini Tanzania Mheshimiwa Saud bin Hilal Alshaidani.
Ujumbe huo pia uliambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Makumbusho ya Taifa Dkt. Oswald Masebo na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga.

 
Akiongea baaada ya kutembelea Kijiji cha Makumbusho Mhe. Al Moosawi alielezea kuridhishwa kwake na uhifadhi wa historia ya makabila ya Tanzania ambayo ameisikia na kuona jinsi nyumba za makabila hayo kama zilivyooneshwa katika eneo hilo na kupongeza jitihada za kuhifadhi historia hiyo kwa ajili ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Kijiji cha makumbusho ni eneo linalohifadhi mifano ya nyumba na vifaa vya makabila na tamaduni mbalimbali zinazopatikana Tanzania.
Eneo hilo lilianzishwa mwaka 1966 kwa ajili ya kuonyesha na kutunza tamaduni za asili, ngoma na tamaduni za makabila mbalimbali kama Wanyakyusa, Wamakonde, Wamasai, Wachagga, Wahaya, Wangoni, Wayao na mengine mengi.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.