Monday, November 13, 2023

WAZIRI MAKAMBA AWASILI UHOLANZI KWA ZIARA YA KIKAZI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akielezea juu ya ushiriki wa ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Novemba 2023 jijini The Hague, Uholanzi. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida na kushoto ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano waTanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Yusuf Makamba (Mb.) amewasili Jijini The Hague, Uholanzi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu (3) kuanzia tarehe 13 - 15 Novemba 2023. 

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Makamba ataongoza ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji Kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Jijini The Hague.

Aidha, pembezoni mwa kongamano hilo, Mhe. Waziri Makamba atapata nafasi ya kukutana na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Mhe. Kanke Bruins Slot. Kadhalika, Mhe. Makamba anatarajiwa pia kukutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Uholanzi (Tanzania Diaspora).

Waziri Makamba ameambatana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Daniel Mushi. Wengine wanaoshiriki kwenye ujumbe wa Mhe. Waziri ni Mabalozi na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Pamoja na Wakuu wa Mashirika mbalimbali Serikalini yanayotafuta ubia na mashirika ya Uholanzi. 

Aidha ujumbe wa Waziri Makamba umehusisha wafanyabiashara 16 kutoka sekta binafsi za Tanzania ambao wanashiriki kwenye kongamano hilo.
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Biashara za Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi, Balozi John Ulanga akifafanua masuala mbalimbali yatakayojiri wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (kushoto) na kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya mifugo), Dkt. Daniel Mushin a wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga.
Viongozi Waandamizi kutoka sekta ya umma na binafsi walioambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) nchini Uholanzi wakifatilia ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha ndani cha maandalizi.
Viongozi Waandamizi kutoka sekta ya umma na binafsi walioambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) nchini Uholanzi wakifatilia ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha ndani cha maandalizi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Amsterdam, Uholanzi tarehe 13 Novemba 2023
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akielezea juu ya ushiriki wa ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Novemba 2023 jijini The Hague, Uholanzi. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida na kushoto ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano waTanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta

Sunday, November 12, 2023

TANZANIA NA FINLAND KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO KUMUENZI HAYATI AHTISAARI


Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano na Finland ili kuenzi misingi mizuri ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili iliyowekwa na aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Hayati Martti Ahtisaari.


Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipozungumza katika hafla ya kumbumbuku ya kumuenzi Hayati Ahtisaari  iliyofanyika jijini Helsinki Finland tarehe 11 Novemba 2023.


Amesema Hayati Ahtisaari ambaye dunia inamtambua kwa mchango wake mkubwa katika kutetea amani, Tanzania itaendelea kumuenzi na kutambua mchango wake mkubwa alioutoa katika kuimarisha ushirikiano na Tanzania tangu akiwa Balozi wa Finland nchini Tanzania mwaka 1973 hadi 1976 na alipokuwa Rais wa nchi hiyo mwaka 1994 hadi 2000.

Amesema kupitia misingi hiyo,   Finland imekuwa mshirika mzuri wa Tanzania katika kutekeleza agenda mbamlimbali  za maendeleo na kwamba mchango wa nchi hiyo  kwenye sekta mbalimbali za maendeleo utaendelea kubaki kama alama ya kukumbukwa tangu Tanzania ilipotoka na ilipo sasa.


“Ninayo furaha kusema kwamba, Serikali ya Tanzania chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuhakikisha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizi mbili na watu wake unaimarika siku hata siku” alisisitiza Mhe. Balozi Mbarouk.



Vilevile amesema kuwa, mtazamo wa Tanzania na Filand katika agenda  mbalimbali za kimataifa unafanana, hivyo Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi hiyo kuhakikisha agenda hizo  ikiwemo kuleta maendeleo ya kiuchumi duniani, ulinzi wa amani na mapambano dhidi ya umaskini zinatekelezwa ili kuifanya dunia mahali salama pa kila mmoja kuishi.


Kadhalika Mhe. Balozi Mbarouk amepongeza kuwepo kwa Mfuko wa Amani wa Martti Ahtisaari (CMI) ambao una jukumu kubwa la kuendelea kuenzi urithi mwema aliouacha Hayati Ahtisaari ambaye anatambulika kama mtetezi bingwa wa Amani duniani.



Mhe. Balozi Mbarouk alitoa hotuba hiyo kwa  niaba ya Rais Mstaafu,  Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete ambaye alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye mazishi ya kitaifa ya Hayati Ahtisaari yaliyofanyika jijini Helsiknki tarehe 10 Novemba 2023. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akihutubia wakati wa hafla maalum ya kumbukumbu kumuenzi aliyekuwa Rais Mstaafu wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari iliyofanyika jijini Helsinki, Finland tarehe 11 Novemba 2023. Mhe. Balozi Mbarouk alitoa hotuba hiyo kwa niaba ya Rais Mstaafu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwenye mazishi ya Hayati Ahtisaari yaliyofanyika jijini hapo tarehe 10 Novemba 2023

Mhe. Balozi Mbarouk akiendelea na hotuba yake, ambapo pamoja na mambo mengine alisema Tanzania itaimarisha ushirikiano na Finland kumuenzi Hayati Ahtisaari


Mhe. Balozi Mbarouk akihutubia


 

Saturday, November 11, 2023

KIKWETE AMWAKILISHA RAIS SAMIA KWENYE MAZISHI YA RAIS WA ZAMANI WA FINLAND


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya Mazishi ya Kitaifa ya Rais wa Zamani wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari iliyofanyika Helsinki tarehe 10 Novemba 2023. 

Wakati wa kutoa salamu za pole, Rais Kikwete alisema kuwa Rais Samia anatoa salamu za rambirambi kwa Rais wa Findland, Mhe. Sauli Niinistö, Familia ya Marehemu na watu wote wa Finland kufuatia kifo cha kiongozi huyo mashuhuri duniani.

Rais Kikwete aliungana na viongozi mbalimbali walioshiriki mazishi hayo wakimwemo Rais wa Kosovo, Mhe. Vyosa Osmani na Rais wa Namibia, Mhe. Hage Geingob na kummwagia sifa Hayati Martti Ahtisaari kwamba alikuwa kiongozi mwenye maono na mpenda amani duniani.

Hayati Martti Ahtisaari aliwahi kuwa Balozi wa Finland nchini Tanzania kuanzia mwaka 1973 hadi 1976 na alikuwa Rais wa Finland kuanzia mwaka 1994 hadi 2000. Katika vipindi vyote hivyo, Hayati Martti Ahtisaari aliimarisha uhusiano wa Tanzania na Finland katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya ziara ya kitaifa nchini Tanzania mwaka 1997 wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu iliyokuwa inaongozwa na Hayati Benjamin Mkapa.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete akimpa pole Mjane wa Rais wa Zamani wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais wa Finland, Mhe. Sauli Niinistö wakati wa hafla alyoiandaa kwa viongozi na wageni walioshiriki Mazishi ya Kitaifa ya Rais wa zamani wa nchi hyo, Hayati Martti Ahtisaari yaliyofanyika tarehe 10 Novemba 2023.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na viongozi na waombolezaji wengine katika hafla ya mazishi ya kitaifa ya Rais wa Zamani wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari iliyofanyika Helsinki tarehe 10 Novemba 2023. Rais Kikwete alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi hayo.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na viongozi na waombolezaji wengine katika hafla ya mazishi ya kitaifa ya Rais wa Zamani wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari iliyofanyika Helsinki tarehe 10 Novemba 2023. Rais Kikwete alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi hayo
Hafla ya Mazishi ya Kitaifa ya Rais wa Zamani wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari ikiendelea Helsinki tarehe 10 Novemba 2023 

Wednesday, November 8, 2023

MAPENDEKEZO YA TUME YA HAKI JINAI NCHINI YAANZA KUTEKELEZWA

Kamati ya Kusimamia utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Kurekebisha Mifumo ya Haki Jinai nchini imekutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wanaowakilisha nchi na taasisi zao nchini.

Kamati hiyo imewahakikishia Mabalozi na wawakilishi hao kuwa baadhi ya mapendekezo yameanza kufanyiwa kazi na Serikali.

Akizungumza na mabalozi na wawakilishi hao kuwapa mrejesho wa taarifa ya tume ya kuboresha muundo wa taasisi za haki jinai Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Kurekebisha Mifumo ya Haki Jinai, Jaji Mstaafu Mhe. Othman Chande amesema Serikali imeanza kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyowasilishwa na tume hiyo.

Amesema baadhi ya mapendekezo yaliyoanza kutekelezwa ni pamoja na kufunguliwa kwa Ofisi 50 za Mkurugenzi wa Mashitaka katika ngazi ya wilaya nchini ili kusaidia upatikanaji wa haki nchini ikiwa ni moja ya mapendekezo ya kuboresha mfumo wa haki jinai nchini.

Amesema kufunguliwa kwa  ofisi hizo za mashitaka katika wilaya 50 nchini ni jambo lililopendekezwa na tume tangu awali.  

Mhe. Jaji Mustafa Chande alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliunda tume hiyo mwezi Januari 2023 ikiwa na wajumbe tisa na kuipa kazi ya kupitia na kutoa mapendekezo ya kuboresha mfumo wa taasisi za haki jinai nchini kazi iliyokamilika na kuwasilishwa mwezi Julai 2023.

Aliongeza kuwa baada ya kupokea mapendekezo zaidi ya 360 ya tume hiyo yaliyolenga kuboresha taasisi za haki jinai, aliibadilisha tume hiyo na kuwa Kamati ya Kusimamia Utekelezaji wa mapendekezo hayo na kusaidia Serikali kuandaa mpango wa utekelezaji  wa mapendekezo hayo.

Akizungumza katika kikao hicho, Kiongozi wa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na Balozi wa Visiwa vya Comoro, Dkt. Ahamada El Badaoui alisema kazi iliyofanywa na tume ni njema na wao kama mabalozi wanaunga mkono juhudi za serikali katika kutoa haki na kuahidi kuendelea kutoa mchango wao wa ushirikiano na Tanzania.

Naye Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Hamisu Umar Takamawa ameipongeza Kamati kwa kufanya kazi ndani ya muda mfupi na kuja na mapendekezo ambayo ni mazuri na kusema Tanzania ikiyatekeleza  itapiga hatua zaidi na kusema Nigeria wana cha kujifunza kupitia tume hiyo.

“Tumefarijika na taarifa hii, kwa kweli Nigeria tutakuja kuiga mfano huu wa kutekeleza haki jinai hapa Tanzania,” Alisema Balozi Takamawa 

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF), Bi. Shalini Bahuguna ameipongeza tume kwa kuweka mapendekezo ya kuboresha haki za mtoto na kueleza kuwa UNICEF ipo tayari kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika kuhakikisha haki za mtoto zinalindwa na kuimarishwa zaidi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Kurekebisha Mifumo ya Haki Jinai, Jaji Mstaafu Mhe. Othman Chande akizungumza na na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wanaowakilisha nchi na taasisi zao nchini

Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Kurekebisha Mifumo ya Haki Jinai, Jaji Mstaafu Mhe. Othman Chande akikabidhi ripoti ya Tume kwa Kiongozi wa  Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na Balozi wa Visiwa vya Comoro, Dkt. Ahamada El Badaoui. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo.

Kiongozi wa  Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na Balozi wa Visiwa vya Comoro, Dkt. Ahamada El Badaoui akizungumza wakati wa Mabalozi wakipatiwa taarifa ya tume ya kuboresha muundo wa taasisi za haki jinai Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia kikao 

Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Tri Yogo Jatmiko akichangia jambo wakati wa Mabalozi wakipatiwa taarifa ya tume ya kuboresha muundo wa taasisi za haki jinai Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akizungumza kwenye kikao hicho



BALOZI MBAROUK AMUAGA BALOZI WA AUSTRALIA

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) amemuaga Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake nchini Kenya, Mhe. Luke Williams baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi.

Akizungumza na Mhe. Balozi Williams walipokutana katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam, Waziri Mbarouk amesema Tanzania na Australia zimekuwa na uhusiano mzuri uliowezesha mataifa hayo kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta za elimu, utalii, madini, nishati, mabadiliko ya tabia nchi, pamoja na biashara na uwekezaji. 

Waziri Mbarouk ameongeza kuwa ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Australia ni jambo lililochochewa na kazi nzuri iliyofanywa na Balozi Williams wakati akitekeleza majukumu yake ya kibalozi.

“Katika kipindi chako umeiwakilisha vyema Australia na kuonesha mafanikio makubwa ambayo yamefikiwa kati ya Tanzania na Australia. 

Kazi yako imechochea uboreshaji wa sekta za elimu, utalii, madini, nishati, uchumi wa buluu na kuchangia ukuaji wa sekta ya biashara uwekezaji katika nchi zetu, ni matumaini yangu kuwa utaendelea kuwa Balozi mwema kwa Tanzania nchini Australia na kokote uendako Duniani,” amesema Balozi Mbarouk.

Balozi Mbarouk ameongeza kuwa Australia imekuwa ikitoa fursa za ufadhili wa masomo katika sekta mbalimbali, ila kwa sasa Tanzania inaomba fursa hizo zijikite zaidi katika sekta ya nishati.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Mbarouk amemueleza Balozi Williams kuwa kwa sasa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kiasi kikubwa na kuwaalika wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Australia kuja kuwekeza kwa wingi nchini. 

Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake Nairobi nchini Kenya, Mhe. Luke Williams akizungumza na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake Nairobi nchini Kenya, Mhe. Luke Williams katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake Nairobi nchini Kenya, Mhe. Luke Williams katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake Nairobi nchini Kenya, Mhe. Luke Williams katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.  Balozi Williams amemaliza muda wake wa uwakilishi.

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Balozi wa Australia nchini mwenye makazi yake Nairobi nchini Kenya, Mhe. Luke Williams katika picha ya pamoja na watumishi kutoka Ubalozi wa Australia na Wizara katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam





DIPLOMASIA YA UCHUMI NI UTEKELEZAJI WA SERA YA MAMBO YA NJE- BYABATO


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb) amesema Diplomasia ya uchumi ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayojumuisha mipango na mikakati ili kunufaisha taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa unaofanyika kupitia ushirikiano baina ya Tanzania, mataifa mbalimbali, jumuiya za kikanda na za kimataifa.

Amesema utekelezaji huo unajumuisha utafutaji wa masoko nje ya nchi, kuvutia uwekezaji, biashara, watalii, kutafuta mikopo ya fedha ya masharti nafuu, ufadhili wa masomo nje ya nchi na uhaulishaji wa teknolojia za kisasa ambazo hutumiwa na sekta za uzalishaji zikiwemo viwanda, kilimo na nishati. 

Mhe. Byabato ameongeza kuwa katika kutekeleza diplomasia ya uchumi Tanzania inapata mapinduzi makubwa ya sayansi na teknolojia na kuchangia maendeleo ya Taifa na kufafanua kuwa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Marekani inakamilisha taratibu za ujenzi wa kiwanda cha kuchakata madini ya kutengenezea betri za magari ya umeme kinachotarajiwa kukamilika mwaka 2026. 

“Kiwanda hiki kitaleta teknolojia mpya ya utengenezaji wa vifaa vya magari, kuhaulisha teknolojia nchini na kuibua vipaji vipya kwa vijana watakaopata ajira katika Kiwanda hicho,” alisema Mhe. Byabato. 

Amesema diplomasia ya uchumi inasaidia upatikanaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania nje ya nchi na kuongeza kuwa hadi kufikia mwezi Septemba, 2023 Tanzania imeuza tani 13,708 za nyama ikilinganishwa na tani 1,777 zilizouzwa mwaka 2020/21. 

“Masoko hayo yamepatikana katika nchi za China, Kuwait, Oman, Qatar, Vietnam na Umoja wa Falme za Kiarabu, masoko haya yamechochea sekta ya uzalishaji kwa ujumla wake,” alisisitiza Mhe. Byabato.

Mhe. Byabato alikuwa akijibu swali Bungeni lililoulizwa na Mbunge wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Ameir Abdallah Ameir aliyetakla kujua mchango wa diplomasia ya uchumi katika kuleta mapinduzi ya Sayansi na Teknolojia na sekta za uzalishaji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifafanua jambo wakati akijibu swali Bungeni
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akijibu swali Bungeni 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akisikiliza swali Bungeni
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifafanua jambo wakati akijibu swali Bungeni
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifafanua jambo wakati akijibu swali Bungeni

Saturday, November 4, 2023

RAIS SAMIA APONGEZA UAMUZI WA SADC KUPELEKA MISHENI YA ULINZI WA AMANI NCHINI DRC



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa, Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema, Rais wa Angola Mhe. João Lourenço, Rais wa Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Félix Tshisekedi pamoja na Viongozi mbalimbali kabla ya kuanza kwa Mkutano wa dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika SADC jijini Luanda, Angola 

Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wameazimia kupeleka Misheni ya Ulinzi wa Amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (SAMIDRC) kushughulikia masuala muhimu yanayoathiri utulivu na amani nchini humo kufuatia mapigano ya muda mrefu baina ya makundi ya waasi yenye silaha. 

Azimio hilo limefikiwa kwenye Mkutano wa dharura wa Wakuu wa nchi na Serikali wa SADC uliofanyika jijini Luanda, Angola tarehe 04 Novemba 2023. 

Akizungumza katika Mkutano Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ameeleza kuridhishwa kwake na kupongeza namna Jumuiya hiyo inavyothamini umuhimu wa kuimarisha hali ya ulinzi na usalama, na kuongeza kuwa hatua hiyo ni uthibitisho tosha wa kwamba kanda inaenzi misingi na malengo ya kuanzishwa kwake. 

Awali akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano huo Rais wa Angola Mheshimiwa João Manuel Gonçalves Lourenço na Mwenyekiti wa SADC alieleza kuwa sasa ni wakati muafaka wa kanda hiyo kuhakikisha kuwa DRC inapata amani na utulivu ambao imeukosa kwa muda mrefu.

Aliongeza kusema machafuko hayo yamesababisha vifo vya watu wasio na hatia, familia kufarakana kwa kukimbia machafuko na uharibifu wa mali, hivyo kuwakosesha wananchi nafasi ya kujiletea maendeleo yao na ya kizazi kijacho. 

“Mkutano huu ni muhimu kwa kuwa unaenda kuweka juhudi za pamoja za nchi wanachama wa SADC katika kuleta mabadiliko chanya nchini DRC, ni imani yangu maamuzi yetu yanaenda kuamua mustakabali mwema wa ndugu zetu wa DRC na kuleta matumaini mapya kwa mamilioni ya watu ambao kwa muda mrefu wamekuwa na uhitaji wa utulivu na amani ya kudumu” Alisema Rais Lourenço.

Kwa upande wake Rais wa Zambia Mheshimiwa Hakainde Hichilema ambaye pia ni mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC (Organ Troika) akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa kilele wa Asasi hiyo uliofanyika awali, alieleza kuwa kuimarika kwa usalama wa DRC kutaleta tija katika eneo lote la Kusini mwa Afrika na Afrika kwa ujumla wake. 

“Tunaamini kuwa DRC imara na salama itachangia katika ustawi wa amani ya kikanda na kuchochea maendeleo ya kiuchumi hivyo, tukiwa kama wanachama wa SADC tunasukumwa na dhamira hiyo ya kutafuta amani na utulivu wa nchini DRC” Alisema Rais Hichilema

Katika hatua nyingine mkutano huo wa Wakuu wa Nchi umetoa wito kwa mashirika yanayojihusisha na utoaji wa misaada mbalimbali ya kibinadamu kuendelea kutoa mahitaji muhimu kwa raia wa DRC wanaothiriwa na machafuko yanayoendelea nchini humo ikiwemo chakula, malazi na matibabu. 

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliohudhuriwa na nchi 12 umehitimishwa leo Novemba 4, 2023 jiijini Luanda, Angola. Mkutano huo ulitanguliwa na mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama na Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu na Mawaziri kilichofanyika tarehe 3 Novemba 2023. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa (kushoto) Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema (kulia) katika picha ya moja muda mfupi kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika SADC jijini Luanda, Angola

Friday, November 3, 2023

TANZANIA YANUFAIKA KUTOA WALINZI WA AMANI KATIKA MISHENI ZA UMOJA WA MATAIFA

 

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) akijibu swali Bungeni


 

 


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) ameliambia Bunge kuwa ushiriki wa Tanzania katika Misheni za Ulinzi wa Amani umekuwa na manufaa mbalimbali kwa Taifa ikiwemo mafunzo ya ziada na ajira za kiraia kwa watanzania.


Mhe. Balozi Mbarouk alitoa kauli hiyo Bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe. Cosato Chumi aliyetaka kujua Tanzania inanufaika kiasi gani katika uuzaji wa bidhaa na huduma katika maeneo ambayo Jeshi la Tanzania linafanya ulinzi wa amani.

Balozi Mbarouk amesema kuwa Tanzania imeendelea kuwa mstari wa mbele katika  kushiriki kwenye jitihada mbalimbali za kutafuta amani duniani kama ilivyoainishwa katika Sera ya Mambo ya Nje 2001 na yapo manufaa makubwa katika ushiriki huo.


“Ushiriki wa Tanzania katika Misheni za Ulinzi wa Amani umekuwa na manufaa mbalimbali ikiwemo; Walinda amani wetu kufaidika na mafunzo ya ziada ambayo yanawajenga na kuwaimarisha,” alisema Balozi Mbarouk

Ametaja faida nyingine nchi inayopata kuwa ni pamoja na ajira za kiraia kwa watanzania na kudumisha utamaduni hususan kukua kwa lugha ya Kiswahili na kutolea mfano katika eneo la DRC, Lebanon na Darfur kumekuwa na ongezeko la matumizi ya lugha ya Kiswahili.

Mhe. Balozi Mbarouk amesema mbali na manufaa yaliyoainishwa, zipo fursa za kiuchumi ambazo nchi inazipata katika shughuli za ulinzi wa amani.

Balozi Mbarouk ametaja fursa hizo kuwa ni biashara ya bidhaa zinazotumiwa na vikosi vilivyopo katika Misheni kama chakula, mavazi, vinywaji, vifaatiba na dawa.

“Fursa nyingine ni usafirishaji wa mizigo, ujenzi wa majengo yanayohamishika, vifaa na huduma za TEHAMA na kuongeza kuwa Tanzania inaweza pia kuuza teknolojia ya kutumia panya katika kubaini na kutegua mabomu yaliyotegwa ardhini kama fursa za kiuchumi”, alisema Mhe. Balozi Mbarouk.

WAKUU WA NCHI ZA SADC KUKUTANA KWA DHARURA ANGOLA


 

Wednesday, November 1, 2023

UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUBORESHA MAKUMBUSHO YA MAJIMAJI

Serikali ya Ujerumani imeahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuboresha Makumbusho ya Majimaji ili  kuhifadhi kumbukumbu sahihi kwa ajili ya wakati huu na kwa  vizazi vijavyo.

Ahadi hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier alipotembelea Makumbusho ya Vita vya Maji Maji  Songea Mkoani Ruvuma.

Mhe., Dkt. Steinmeier amesema Ujerumani ipo tayari kufanya uchambuzi na mchakato wa historia ya vita vya Maji Maji kwakuwa kilichotokea zamani hakipaswi kusauhilka na mtu yoyote.

“Ili kuweka kumbukumbu sawa kwa sasa na kwa wakati ujao, Ujerumani tunaahidi kushirikiana na Tanzania kuboresha makumbusho hii,” alisisitiza Mhe. Rais Steinmeier. 

Mhe. Dkt. Steinmeier alisema Ujerumani inatamani kufanya uchambuzi na mchakato wa historia ya ‘Vita vya Maji Maji’ na kuongeza kuwa mchakato huo utahusisha vijana, wanafunzi wa shule na vyuo vikuu, wasomi na wataalamu wa hifadhi na sehemu za kumbukumbu. 

“Mwaka 2024, Ujerumani inampango wa kufanya maonesho kwa kushirikiana na Makumbusho ya Taifa ya Tanzania, maonesho hayo yatajulikana kwa jina la  “Historia ya Tanzania”, alisema Mheshimiwa Steinmeier. 

Awali Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Mb.) alisema historia ya Tanzania na Ujerumani ina sura mbili tofauti. Alifafanua kuwa sura ya kwanza ni kuhusu vita waliyopigana babu zetu na sura ya pili ni yale mazuri yaliyofanywa na Serikali ya Ujerumani Kama vile kujenga shule, hospitali na kutoa huduma nyingine za kijamii.

“Muhimu zaidi ni kukumbuka na kusahau yaliyopita na kuendelea kudumisha uhusiano mzuri uliopo na kusonga mbele kwa kuleta maendeleo kati ya mataifa yetu mawili, lakini pia katika mji wetu wa Songea ,” alisema Dkt. Ndumbaro

Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa Songea wanatamani kuona makumbusho ya kisasa ya ushirikiano kati ya Ujerumani na Tanzania yakijengwa Songea, “pia tunatamani Ujerumani itusaidie kuboresha chuo cha VETA Songea ili kuwawezesha vijana wetu kupata mafunzo mbalimbali,” alisema Dkt. Ndumbaro.

Waziri Ndumbaro pamoja na mambo mengine, ameiomba Serikali ya Ujerumani kushirikiana na Mji wa Songea kwa kuwawezesha kutembeleana, kushirikiana na kuendeleza utani kati ya Wangoni na Wajerumani.

Mheshimiwa Rais Stenmeier mbali na kutembelea Makumbusho ya Vita vya Maji Maji pia ametembelea Shule ya Msingi ya Majimaji. 

Makumbusho ya Vita vya Maji Maji ni makumbusho pekee nchini Tanzania inayoonesha historia kubwa ya Vita vya Maji Maji katika harakati za ukombozi dhidi ya ukoloni wa Wajerumani.

Mheshimiwa Rais Stenmeier amehitimisha ziara yake ya Kikazi ya siku tatu nchini leo tarehe 01 Novemba 2023.

Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier akipokelewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro katika Uwanja wa Ndege wa Songea  kutembelea Makumbusho ya Vita vya Maji Maji Wilayani Songea Mkoani Ruvuma

Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier akiweka shada la maua katika kaburi la walilozikwa mashujaa wa Vita vya Maji Maji
Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier akiweka ua katika kaburi la Chifu Nduna 

Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier akiwa amekaa na wanafunzi wa shule ya Msingi Maji Maji alipofanya ziara shuleni hapo 




Tuesday, October 31, 2023

BALOZI MBAROUK AMPONGEZA DKT. TULIA KWA USHINDI URAIS IPU

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson.

Balozi Mbarouk aliambatana na Mabalozi watatu  (3) waliohusika kwenye Kampeni ya IPU walipoenda kumpongeza kwa ushindi huo na kumhakikishia Ushirikiano wa Wizara katika utekelezaji wa Majukumu yake Mapya.

Mabalozi watatu ni pamoja na  Naibu Mwakilishi wa Kudumu, Uwakilishi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Seiman Suleiman, Naibu Mwakilishi wa Kudumu, Uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Geneva, Balozi Hoyce Temu pamoja na Balozi Robert Kahendaguza.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson katika Ofisi za Bunge Dodoma

Mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson yakiendelea katika Ofisi za Bunge Dodoma

Mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson yakiendelea katika Ofisi za Bunge Dodoma

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson katika Ofisi za Bunge Dodoma

Picha ya Pamoja