Sunday, November 12, 2023

TANZANIA NA FINLAND KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO KUMUENZI HAYATI AHTISAARI


Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano na Finland ili kuenzi misingi mizuri ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili iliyowekwa na aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Hayati Martti Ahtisaari.


Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipozungumza katika hafla ya kumbumbuku ya kumuenzi Hayati Ahtisaari  iliyofanyika jijini Helsinki Finland tarehe 11 Novemba 2023.


Amesema Hayati Ahtisaari ambaye dunia inamtambua kwa mchango wake mkubwa katika kutetea amani, Tanzania itaendelea kumuenzi na kutambua mchango wake mkubwa alioutoa katika kuimarisha ushirikiano na Tanzania tangu akiwa Balozi wa Finland nchini Tanzania mwaka 1973 hadi 1976 na alipokuwa Rais wa nchi hiyo mwaka 1994 hadi 2000.

Amesema kupitia misingi hiyo,   Finland imekuwa mshirika mzuri wa Tanzania katika kutekeleza agenda mbamlimbali  za maendeleo na kwamba mchango wa nchi hiyo  kwenye sekta mbalimbali za maendeleo utaendelea kubaki kama alama ya kukumbukwa tangu Tanzania ilipotoka na ilipo sasa.


“Ninayo furaha kusema kwamba, Serikali ya Tanzania chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuhakikisha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizi mbili na watu wake unaimarika siku hata siku” alisisitiza Mhe. Balozi Mbarouk.



Vilevile amesema kuwa, mtazamo wa Tanzania na Filand katika agenda  mbalimbali za kimataifa unafanana, hivyo Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi hiyo kuhakikisha agenda hizo  ikiwemo kuleta maendeleo ya kiuchumi duniani, ulinzi wa amani na mapambano dhidi ya umaskini zinatekelezwa ili kuifanya dunia mahali salama pa kila mmoja kuishi.


Kadhalika Mhe. Balozi Mbarouk amepongeza kuwepo kwa Mfuko wa Amani wa Martti Ahtisaari (CMI) ambao una jukumu kubwa la kuendelea kuenzi urithi mwema aliouacha Hayati Ahtisaari ambaye anatambulika kama mtetezi bingwa wa Amani duniani.



Mhe. Balozi Mbarouk alitoa hotuba hiyo kwa  niaba ya Rais Mstaafu,  Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete ambaye alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye mazishi ya kitaifa ya Hayati Ahtisaari yaliyofanyika jijini Helsiknki tarehe 10 Novemba 2023. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akihutubia wakati wa hafla maalum ya kumbukumbu kumuenzi aliyekuwa Rais Mstaafu wa Finland, Hayati Martti Ahtisaari iliyofanyika jijini Helsinki, Finland tarehe 11 Novemba 2023. Mhe. Balozi Mbarouk alitoa hotuba hiyo kwa niaba ya Rais Mstaafu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwenye mazishi ya Hayati Ahtisaari yaliyofanyika jijini hapo tarehe 10 Novemba 2023

Mhe. Balozi Mbarouk akiendelea na hotuba yake, ambapo pamoja na mambo mengine alisema Tanzania itaimarisha ushirikiano na Finland kumuenzi Hayati Ahtisaari


Mhe. Balozi Mbarouk akihutubia


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.