Thursday, November 16, 2023

RAIS WA ROMANIA AWASILI NCHINI


Rais wa Romania, Mheshimiwa Klaus Iohannis, amewasili nchini kwa ziara ya Kitaifa kuanzia leo tarehe 16 hadi 19 Novemba 2023 kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere amepokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb.)

Lengo la ziara hiyo ni pamoja na kushawishi uwekezaji zaidi na kuvutia watalii wengi kutoka nchini Romania.

Aidha katika mazungumzo rasmi yatakayofanyika tarehe 17 Novemba 2023 Rais huyo na mwenyeji wake watajadili namna bora ya kukuza na kuimarisha ushirikiano kati sekta za elimu, afya, kilimo nishati na madini.

Kabla ya kuondoka nchini tarehe 19 Novemba 2023 Rais wa Romania atapata fursa ya kwenda Zanzibar ambapo atazungumza na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi na kutembelea Mji Mkongwe ambao ni moja kati ya vivutio vikubwa vya utalii duniani
Rais wa Romania Mheshimiwa Klaus Iohannis akiwapungia wananchi waliojitokeza kumlaki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais wa Romania, Mheshimiwa Klaus Iohannis akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb.) alipompokea wakati akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)

Rais wa Romania, Mheshimiwa Klaus Iohannis kizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb.)  alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam

Rais wa Romania, Mheshimiwa Klaus Iohannis kizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb.)  alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam
Rais wa Romania, Mheshimiwa Klaus Iohannis akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samuel Shelukindo alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.